" Kumekucha: CCM Yapiga Marufuku Kuchukua Form na Misafari ya Wapambe

Kumekucha: CCM Yapiga Marufuku Kuchukua Form na Misafari ya Wapambe

 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa mwongozo na maelekezo kwa umma kuhusu utaratibu wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu kwa Wanachama wa CCM wanaoomba kuteuliwa kugombea uongozi katika vyombo vya dola 2025 kuanzia June 28,2025 ambapo kimepiga marufuku kwa Mwanachama yeyote kualika kundi la Wapambe kumsindikiza kwenda CCM kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea.

Taarifa iliyotolewa leo June 25,2025 na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Issa Haji (Gavu) imesema ni marufuku pia kwa Mwanachama kuandaa msafara wa magari, pikipiki, baiskeli, ngoma na matarumbeta ya kumsindikiza kwenda CCM kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea ambalo lengo la kupiga marufuku mbwembwe hizo ni kusimamia na kulinda misingi ya Chama katika kuwaunganisha Wanachama wake, Chama hakina budi kuimarisha umoja, upendo, ushirikiano, na mshikamano.

“CCM inakumbusha Viongozi, Watendaji na Wanachama kuendelea kufuata maadili ya uchaguzi kama ilivyoanishwa kwenye Katiba, Kanuni za Uchaguzi wa CCM na Miongozo yake” imeeleza taarifa hiyo.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post