Na Mapuli Kitina Misalaba
Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kulinda na kutunza mazingira,
akisisitiza kuwa suala hilo ni jukumu la kila mmoja kwa ustawi wa jamii ya sasa
na vizazi vijavyo.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya
Mazingira Duniani yaliyofanyika leo Juni 5, 2025 katika maeneo mbalimbali
Manispaa ya Shinyanga ambayo yameambatana na zoezi la kufanya usafi katika
maeneo ya soko la Ngozonane, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utamaduni wa usafi
na uhifadhi wa mazingira kwa vitendo.
“Jambo la mazingira ni letu sote, kila mmoja anahusika. Tunatakiwa
tuhifadhi mazingira yetu ili na sisi yaweze kutuhifadhi, tutunze mazingira yetu
ili na sisi yaweze kututunza, ikiwa ni pamoja na kupanda miti, tusikate miti
ovyo.”amesema Zamda.
Ameongeza kuwa kufanya usafi mara kwa mara si tu
kunalinda mazingira bali pia kunachangia katika afya bora za wananchi:
“Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mazingira
safi na maisha bora ya mwanadamu. Wazazi wetu walitupandia miti na kutuachia
mazingira rafiki; nasi tuendelee kupanda miti ili na vizazi vyetu vipate
mazingira bora ya kuishi.”amesema Zamda
Kwa upande wake, Mkuu
wa Idara ya Mazingira na Maliasili wa Manispaa ya Shinyanga, Ezra Manjerenga,
amesema serikali inasisitiza wananchi kuwajibika katika kutunza mazingira
sambamba na kudhibiti matumizi ya plastiki.
Ameongeza kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamebeba
ujumbe mzito wa kuhimiza jamii kuchukua hatua sasa.
“Ujumbe wetu mwaka huu unatusisitiza cha kwanza tuwe
na wajibu wa kutunza na kuhifadhi mazingira ili tuwe na haki ya kuyatumia
mazingira yetu. Lakini la pili ni matumizi na udhibiti wa plastiki, kwa hiyo
ujumbe wetu pia ni kuhakikisha tunakuwa na matumizi salama na endelevu ya
plastiki,” amesema Manjerenga.
Amesema kaulimbiu ya
mwaka huu ni:
“Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo Tuwajibike Sasa;
Dhibiti Matumizi ya Plastiki,” ambayo inalenga kuelimisha umma
kuhusu madhara ya taka zisizooza na kuhimiza matumizi ya mifuko mbadala.
Baadhi ya wakazi wa
Manispaa ya Shinyanga waliohudhuria maadhimisho hayo wameeleza kufurahishwa na
ushiriki wao katika shughuli za utunzaji wa mazingira, wakisisitiza kuwa ni
jukumu la kila mmoja kuhakikisha anahifadhi mazingira kwa manufaa ya sasa na
baadaye.
Wamesema utunzaji wa mazingira unasaidia kuzuia
magonjwa, kuboresha mandhari ya maeneo ya makazi na kusaidia kupambana na
athari za mabadiliko ya tabianchi.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.








Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akiongoza maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika
leo Juni 5, 2025 mjini Shinyanga.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akiongoza maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika
leo Juni 5, 2025 mjini Shinyanga.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akiongoza maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika
leo Juni 5, 2025 mjini Shinyanga.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda
Shaban Mwebea, akiongoza maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika
leo Juni 5, 2025 mjini Shinyanga.
Post a Comment