

Na Mapuli Kitina
Misalaba
Wadau kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wamekutana
leo Julai 9, 2025 katika ukumbi wa Redio Faraja FM kushiriki mjadala maalum
kuhusu malezi na makuzi ya mtoto, ulioandaliwa na Redio Faraja kwa kushirikiana
na shirika la ICS – Investing in Children and Strengthening their Societies (Creating
Change).
Mjadala huo ambao pia
umetangazwa mubashara kupitia Redio Faraja na kurasa zake za mitandao ya
kijamii, umejumuisha washiriki kutoka Umoja wa Wanaume Mkoa wa Shinyanga,
viongozi wa dini, viongozi wa Serikali za mitaa, viongozi wa kimila, wataalamu
wa ustawi wa jamii, watoto, wazazi na walezi pamoja na wawakilishi kutoka
taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali.
Katika mjadala huo,
washiriki wamechangia maoni na uzoefu juu ya namna jamii inavyoweza kushirikiana
kwa pamoja kuhakikisha watoto wanapata malezi bora yanayozingatia haki zao za
msingi kama vile elimu, afya, ulinzi na fursa ya kuishi maisha ya furaha na
usalama.
Afisa Ustawi wa Jamii
wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Lydia Kwesigabo, ameeleza kwa
kina sheria na miongozo mbalimbali inayolinda haki na ustawi wa mtoto,
akisisitiza kuwa malezi ya mtoto ni jukumu la pamoja linalohitaji ushirikiano
wa familia, jamii na serikali.
Naye Afisa Mradi kutoka
ICS, Bi. Lucy Maganga, amesema shirika hilo linaendelea kutekeleza miradi
mbalimbali ya uhamasishaji wa jamii juu ya malezi chanya, kwa kushirikiana na
viongozi wa kimila, wa dini, pamoja na familia, ili kuhakikisha watoto
wanalelewa katika mazingira salama na yenye heshima kwa utu wao.
Akifunga mjadala huo,
mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni mtangazaji wa Redio Faraja FM, Simeo
Makoba, ameishukuru serikali ya mkoa kwa kuruhusu wataalamu wake kushiriki, na
kutoa shukrani maalum kwa Mkuu wa Mkoa Mhe. Mboni Mhita kwa ushirikiano.
Aidha, amelipongeza shirika la ICS kwa kushirikiana
bega kwa bega kufanikisha mjadala huo wenye umuhimu mkubwa kwa ustawi wa watoto
katika jamii ya Shinyanga.
Mjadala huu umeibua
hoja nzito kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakumba watoto ikiwemo ukatili wa
kingono, ndoa za utotoni, kazi ngumu zisizolingana na umri, ukosefu wa elimu
bora, pamoja na migogoro ya kifamilia ambayo huathiri moja kwa moja malezi na
makuzi yao.
Wadau wamehimiza kuanzishwa kwa mikakati endelevu ya
utoaji elimu kwa jamii kuhusu malezi chanya, huku wakitoa rai kwa Serikali na
mashirika yasiyo ya kiserikali kuongeza nguvu katika kulinda haki za watoto.
Kwa kauli moja, washiriki wa mdahalo huu wameafiki kuwa hatima ya mtoto wa leo ndiyo msingi wa taifa la kesho, hivyo ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha mtoto analelewa kwa maadili, upendo na ulinzi unaostahili.
Afisa Mradi kutoka ICS, Bi. Lucy Maganga akizungumza
kwenye mjadala maalum kuhusu malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika
ukumbi wa Radio Faraja leo Julai 9, 2025.

Afisa Mradi kutoka ICS, Bi. Lucy Maganga akizungumza
kwenye mjadala maalum kuhusu malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika
ukumbi wa Radio Faraja leo Julai 9, 2025.
Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa
wa Shinyanga, Bi. Lydia Kwesigabo, akizungumza kwenye mjadala maalum kuhusu
malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika ukumbi wa Radio Faraja leo
Julai 9, 2025.

Afisa Mradi kutoka ICS, Bi. Lucy Maganga akizungumza
kwenye mjadala maalum kuhusu malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika
ukumbi wa Radio Faraja leo Julai 9, 2025.
Afisa Mradi kutoka ICS, Bi. Lucy Maganga akizungumza
kwenye mjadala maalum kuhusu malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika
ukumbi wa Radio Faraja leo Julai 9, 2025.




Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa
wa Shinyanga, Bi. Lydia Kwesigabo, akizungumza kwenye mjadala maalum kuhusu
malezi na makuzi ya mtoto ambao umefanyika katika ukumbi wa Radio Faraja leo
Julai 9, 2025.

Post a Comment