" MTENDAJI WA KIJIJI AJIUA KWA SUMU YA PANYA - KAHAMA

MTENDAJI WA KIJIJI AJIUA KWA SUMU YA PANYA - KAHAMA

MTENDAJI wa Kijiji cha Ulowa Namba Moja, Kata ya Ulowa, Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Juliana Mkumbo (30) anadaiwa kujiua kwa kunywa sumu ya panya.


Kamanda wa Jeshi la Polisi, Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi huku akieleza baada ya Juliana kutoonekana siku moja nyumbani kwake waligonga mlango kwa muda mrefu lakini haukufunguliwa ndipo ukavunjwa.

Kamanda Magomi alisema walipoingia ndani walimkuta amelala huku matapishi yake yakiwa pembeni na jeshi la polisi lilifika na kuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka hospitali ya Kahama kwa ajili ya uchunguzi na majibu yalibainika kuwa amekunywa sumu ya panya.

“Mwili wake umefanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama na uchunguzi wa awali umebainisha kuwa mtendaji huyo alifariki baada ya kunywa sumu ya panya. Lakini bado tunaendelea na uchunguzi ili kubaini zaidi chanzo cha kifo chake,” alisema Magomi.

Post a Comment

Previous Post Next Post