Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwanamke jasiri
na mwenye ulemavu, Mwajuma K. Mbogo, leo Julai 1, 2025, ameendeleza dhamira yake ya kisiasa kwa
kurejesha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
ili kuwania nafasi ya udiwani katika Kata ya
Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.
Mwajuma, ambaye
alichukua fomu hiyo Juni 29, 2025, amesema kurejesha fomu ni hatua rasmi ya
kuthibitisha kwamba yupo tayari kwa ajili ya kutumikia wananchi wa Ngokolo
endapo chama chake kitamuidhinisha.
"Nimerudisha fomu nikiwa na moyo wa shukrani na
ujasiri. Nimeiva, nina uzoefu, na nina ari ya kuwa sehemu ya mabadiliko chanya
kwa wananchi wa Ngokolo, hasa wanawake na watu wenye ulemavu," amesema Mwajuma mara baada ya kurejesha fomu.
Ameongeza kuwa
hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa
wakati wa kufunga Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo iliyompa msukumo
mkubwa wa kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho, kutokana na namna alivyohimiza
usawa wa kijinsia na ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye nafasi za uongozi.
Kwa mujibu wa
Mwajuma, uzoefu wake katika uongozi unampa ujasiri mkubwa. Ametaja nyadhifa
mbalimbali alizowahi kushikilia, ikiwemo:
·
Mjumbe wa Kamati
ya Ustawi wa Jamii (tawi)
·
Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Wazazi Tawi la Mwadui (2015)
·
Mjumbe wa Kamati
ya Utekelezaji ya UWT tawi la Mwadui
·
Mwenyekiti
Msaidizi wa CHAWATA Wilaya ya Shinyanga
·
Mjumbe wa
SHIVYAWATA Wilaya ya Shinyanga Mjini
"Ulemavu si kikwazo. Tunahitaji kuamini uwezo wa
mtu, si hali yake ya mwili. Nipo tayari kuitumikia Ngokolo kwa uaminifu,
ushirikiano na uwazi,"
amesisitiza Mwajuma.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment