MKURUGENZI WA MANISPAAYA SHINYANGA MWL. ALEXIUS KAGUNZE
WA PILI KUTOKA KUSHOTO MSTARI WA MBELE AKIMKABIDHI BENDERA YA MANISPAA YA
SHINYANGA, MKUU WA MSAFARA WA WANAMICHEZO WA MANISPAA YA SHINYANGA AMBAYE NI
AFISA UTUMISHI HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA NDG. JACOBO
MWAKISU
NA. ELIAS GAMAYA- SHINYANGA.
Akizungumza leo, Agosti 15, 2025, wakati wa kuagana nao kabla ya kuanza safari, Mwl. Kagunze amesema Halmashauri inaimani kubwa sana na wanamichezo hao kufanya vizuri ili kuhakikisha timu hiyo inapata tuzo.
“Nendeni mkaiwakilishe vyema bendera ya Manispaa ya Shinyanga tunamatumaini kubwa sana na nanyi. Kila mmoja wetu twendeni tukashirikiane, tujitume na kupigania ushindi. Ubora tunao, nia tunayo, na shauku ipo sasa ni wakati wa utekelezaji.” amesema Mwl. Kagunze.
Mashindano ya SHIMISEMITA yameanza Agosti 15 na yanatarajiwa kumalizika Agosti 29, 2025, yakihusisha timu kutoka halmashauri mbalimbali nchini.
Post a Comment