" MSHANDETE AJITOSA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SHINYANGA MJINI KUPITIA CHAMA CHA WANANCHI (CUF)

MSHANDETE AJITOSA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SHINYANGA MJINI KUPITIA CHAMA CHA WANANCHI (CUF)

MSIMAMIZI MSAIDIZI WA UCHAGUZI WA JIMBO LA SHINYANGA MJINI, NDG. SAIMON SHOO (kushoto) AKIMKABIDHI FOMU ZA UTEUZI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SHINYANGA MJINI NDG. GERALD MSHANDETE LUBASHA KUPITIA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) (kulia)

                                           NA. ELIAS GAMAYA- SHINYANGA

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Ndg. Saimon Shao leo agosti 19, 2025 amekabidhi fomu za uteuzi mgombea wa nafasi ya Ubunge ndg. Gerald Mshandete Lubasha jimbo la Shinyanga Mjini Kupitia CHAMA CHA WANANCHI (CUF)

 Ndg. Lubasha anakuwa mgombea wa nne kuchukua fomu za Uteuzi  kugombea ubunge kwa jimbo la Shinyanga Mjini ambapo jumla ya vyama 11 vilivyosajiliwa kwa jimbo hili vinatarajiwa kushiriki katika mchakato huo.

 Zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi ya Ubunge umeanza rasmi hapo jana Agosti 14, 2025 ambapo linatarajiwa kutamatika Agosti 27, 2025 ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

 


Post a Comment

Previous Post Next Post