" AZZA HILLAL HAMAD ATAJA VIPAUMBELE VYAKE KWA WANANCHI JIMBO LA ITWANGI

AZZA HILLAL HAMAD ATAJA VIPAUMBELE VYAKE KWA WANANCHI JIMBO LA ITWANGI

Na Mapuli Kitina Misalaba, Picha zote na Kadama Malunde

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Azza Hillal Hamad, ameweka bayana vipaumbele vyake vya maendeleo, akiahidi kupambana kwa nguvu zote kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi wa jimbo hilo zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Akizungumza, katika uzinduzi wa kampeni uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi na viongozi wa CCM, Azza amesema dhamira yake kubwa ni kuhakikisha huduma za kijamii kama afya, maji, kilimo na miundombinu ya barabara zinaboreshwa kwa kiwango kikubwa ili kuinua ustawi wa wananchi.

“Nimekuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa vipindi viwili. Mnanifahamu mimi si mtu wa kupindapinda, mimi ni mtu wa kusema ukweli na kuchukua hatua. Naomba mnitumie, nitahakikisha huduma za afya zinaboreshwa na kukamilisha zahanati na vituo vya afya ambavyo bado havijakamilika, ikiwemo Manyada, Nyida na Butini,” amesema Azza

Akizungumzia sekta ya kilimo, Azza amesema kilimo ndicho uti wa mgongo wa Jimbo la Itwangi, hasa kilimo cha mpunga, na akaahidi kupigania kukamilika kwa Skimu ya Umwagiliaji ya Nyida na miradi mingine ya kilimo inayosuasua.

“Jimbo la Itwangi lina fursa kubwa za kilimo, lakini miradi mingi ya umwagiliaji haijakamilika. Naomba mniamini, nitasimama kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa maslahi ya wakulima na taifa kwa ujumla,” alisema Azza.

Kwa upande wa maji, Azza amesema serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan tayari imetekeleza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria, lakini bado kuna vijiji ambavyo havijafikiwa na huduma hiyo.
“Kuna vijiji 22 vinavyopitiwa na Mradi wa Maji wa Tinde Package ambavyo bado havijapata maji, ikiwemo Kata ya Usanda. Nikichaguliwa, nitahakikisha vijiji hivyo vinapata huduma ya maji safi na salama,” ameahidi Azza.

Azza amewaomba wananchi wa Itwangi kujitokeza kwa wingi tarehe 29 Oktoba 2025 kupiga kura na kuhakikisha ushindi wa CCM kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge hadi Urais.
“Naomba mnipigie kura ili niwatumikie kwa uadilifu na kuhakikisha kila mradi wa maendeleo unakamilika. Pia tumuunge mkono Rais wetu mama Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wetu wote wa CCM,” alisema.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa CCM, Munde Tambwe Abdalla, amesema wananchi wa Itwangi wamepata kiongozi sahihi kwa sababu Azza ni jasiri, mjenga hoja na mtetezi wa wananchi.
“Nawaomba wananchi wa Itwangi, Oktoba 29 mpigie kura Azza Hillal, Rais Dk. Samia na madiwani wote wa CCM ili Jimbo la Itwangi lipate maendeleo ya haraka,” alisema Munde.

Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, amesema Azza ni mchapakazi na mwenye uchungu wa kweli kwa maendeleo ya wananchi, huku Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga, Edward Ngelela, akisisitiza kuwa chama kina imani kubwa na mgombea huyo kutokana na utendaji wake wa kazi.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wameeleza imani yao kwa Azza, wakisema historia yake ya utendaji kazi na kupigania maslahi ya wananchi tangu akiwa Mbunge wa Viti Maalum imewavutia kumchagua.
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 utafanyika Oktoba 29, ambapo wananchi watawachagua madiwani, wabunge na Rais.
Kampeni zimeanza rasmi na CCM inaendelea kusisitiza sera zake za maendeleo kupitia viongozi wake na wagombea katika maeneo mbalimbali ya nchi.


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.
Wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu Jimbo la Itwangi mkoani Shinyanga 
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi, kulia ni Mgeni rasmi Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (MNEC) Munde Tambwe


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.

 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wazazi CCM Taifa, Edwin Peter Nyakanyenge wamemuelezea Azza kama kiongozi wanayemuamini kutokana na historia yake ya kutetea maslahi ya wananchi tangu akiwa Mbunge wa Viti Maalum.
Simon Makoye Mayengo 


Mhandisi Sebastian Malunde.

TAZAMA PICHA MATUKIO YALIYOJIRI
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Munde Tambwe Abdalla akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Itwangi - Picha na Kadama Malunde
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Munde Tambwe Abdalla akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Itwangi
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Munde Tambwe Abdalla akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Itwangi
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Munde Tambwe Abdalla akiwanadi na kuwaombea kura Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad (kulia)na Mgombea Udiwani Kata ya Didia Richard Luhende.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akiwaombea kura wagombea udiwani kata za Jimbo la Itwangi
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akiwaombea kura wagombea udiwani kata za Jimbo la Itwangi
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akiwaombea kura wagombea udiwani kata za Jimbo la Itwangi
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Itwangi CCM Azza Hillal Hamad akinadi sera kwa wananchi.
Mgombea Ubunge wa Vitimaalum Mkoa wa Shinyanga Christina Mzamva akiomba kura za Rais Dk Samia Suluhu Hassan, na Mgombea Ubunge Jimbo la Itwangi 
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wazazi CCM Taifa, Edwin Peter Nyakanyenge akimuombea kura Mgombea wa Ubunge Jimbo la Itwangi, Azza Hillal Hamad
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Ndg. Edward Ngelela akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Jimbo la Itwangi
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Vijijini Ndg. Ernestina Richard akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Jimbo la Itwangi. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Ndg. Edward Ngelela
Abiria kwenye Treni iliyopita eneo la Mkutano wa Kampeni akionesha Bango la Oktoba Tunatiki
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akimuombea Mgombea Urais wa CCM,Rais Dk.Samia Suluhu Hassan,Mgombea Ubunge Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad na Madiwani wote wa CCM.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post