Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu wasaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, Antony Katala na John Maembe, leo Septemba 30,
2025, wamefanya ziara ya kampeni katika Wilaya ya Shinyanga Mjini ambapo
wamekutana na viongozi pamoja na Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya hiyo.
Katika ziara hiyo, viongozi hao wamepata nafasi ya
kuzungumza na kusisitiza mikakati muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Wamewahimiza viongozi na wanachama kuendelea kusaka
kura kwa wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya taifa kwa mgombea urais, Dkt. Samia
Suluhu Hassan, wagombea ubunge pamoja na madiwani wa chama hicho.
Aidha, wamehimiza Kamati ya Utekelezaji kufanya kazi
kwa bidii, mchana na usiku, kuhakikisha CCM na wagombea wake wanapata kura
nyingi za kishindo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Regina Ndulu amesema
jumuiya hiyo ya mkoa imejipanga kuhakikisha maagizo ya viongozi wa taifa
yanatekelezwa kwa vitendo, huku akisisitiza mshikamano wa wanachama na viongozi
wa ngazi zote ili kuongeza kura za wagombea wa CCM.
Akizungumza Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga Mjini, Bi. Doris Kibabi, amewahakikishia viongozi hao kuwa jumuiya
hiyo imejipanga kikamilifu huku akibainisha kuwa wanatarajia kuanza kutembelea makundi
mbalimbali ya wananchi ikiwemo kwenye masoko na minada ili kuwahamasisha kushiriki
kikamilifu katika kupiga kura siku ya uchaguzi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, amesema jumuiya hiyo haitakubali
kuona vitendo vinavyoweza kuharibu mchakato wa uchaguzi huku akiwataka
wanachama kuendelea kushikamana na kuwa wamoja ili kuhakikisha ushindi wa chama
hicho.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji akiwemo Bwana. Leonard Mapolu, amewahakikishia viongozi hao kuwa watayafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na kuendelea kutafuta kura kwa wagombea wa CCM.

Katibu msaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, Antony Katala, akizungumza na jumuiya ya wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga leo Septemba 30, 2025.

Katibu msaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, Antony Katala, akizungumza na jumuiya ya wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga leo Septemba 30, 2025.

Katibu msaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, Antony Katala, akizungumza na jumuiya ya wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga leo Septemba 30, 2025.

Katibu msaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, John Maembe, akizungumza na jumuiya ya wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga leo Septemba 30, 2025.

Katibu msaidizi wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Taifa, John Maembe, akizungumza na jumuiya ya wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga leo Septemba 30, 2025.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, akizungumza.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bi. Doris Kibabi, akizungumza.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bi. Doris Kibabi, akizungumza.
Wajumbe wa kamati ya utekelezaji jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.
Wajumbe wa kamati ya utekelezaji jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment