

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald akizungumza kwenye mahafali hayo ya shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.
Shule ya Msingi Lubaga, iliyopo Manispaa ya Shinyanga,
leo Septemba 19, 2025 imefanya mahafali yake ya 17 kwa wahitimu 64 wa elimu ya
msingi, ambapo hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali, walimu, wazazi,
wanafunzi na wageni waalikwa.
Mgeni rasmi katika mahafali hayo ni Mkurugenzi wa Mamlaka
ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa
na Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA, Nsianel Gerald, ambaye amewapongeza
wahitimu kwa hatua kubwa waliyofikia na walimu kwa malezi na juhudi
walizowekeza katika kuwafundisha na kuwalea watoto hao.
Kwa mujibu wa mkuu wa shule hiyo Mwalimu Stella Lucas
Halimoja amesema Shule ya Msingi Lubaga imeendelea kuwa kinara wa taaluma
katika Manispaa ya Shinyanga ambapo tangu mwaka 2018 hadi sasa, shule imekuwa
ikifaulisha kwa kiwango cha juu cha kati ya asilimia 99 hadi 100, na kwa miaka
minne mfululizo (2021–2024) imekuwa ikishika nafasi ya kwanza kati ya shule za
serikali katika Manispaa.
Amesema mwaka 2018 wanafunzi 73 walihitimu na wote
kufaulu kwa asilimia 100, huku mwaka 2024 wanafunzi 65 pia walihitimu kwa
ufaulu wa asilimia 100 na shule kushika nafasi ya kwanza kiwilaya.
Mwalimu Halimoja ameeleza kuwa matokeo hayo, yamechangiwa
na nidhamu, majaribio ya kila wiki, na mipango ya shule ya kuhakikisha
wanafunzi wanajifunza kwa bidii na kujituma.
Mbali na taaluma, shule imefanikiwa katika nyanja
mbalimbali ikiwemo:
Mpango wa Chakula: Shule imeanzisha mpango wa kupika
chakula na uji shuleni, hatua iliyoimarisha utulivu wa wanafunzi darasani.
Stella amesema Wanafunzi wa madarasa ya mitihani
wamekuwa wakifanya majaribio kila wiki, jambo lililowasaidia kuongeza uelewa na
kujiandaa vizuri kwa mitihani.
Ametumia nafsi hiyo kueleza mafanikio mbalimbali katika
shule hiyo ikiwemo kufanikisha Ujenzi wa choo cha walimu, choo cha wasichana
chenye matundu matano, chumba cha kujihifadhi kwa wanafunzi wa kike, na vyumba
viwili vya madarasa.
Aidha amesema kupitia kamati ya shule na Ofisi ya
Diwani, jamii imesaidia kukamilisha ujenzi wa madarasa mapya yaliyokamilika kwa
asilimia 85, pia Shule imepata mashine ya kudurufu nyaraka kupitia msaada wa
mlezi wa shule, Ndugu Gillio Makula, hatua iliyorahisisha utoaji wa mitihani na
majaribio.
Pamoja na mafanikio hayo, shule inakabiliwa na
changamoto kadhaa zikiwemo ukosefu wa madirisha ya vioo na viti kwenye ofisi
ndogo ya shule, uchakavu wa nyumba ya mwalimu, na hitaji la upakaji rangi
kwenye baadhi ya majengo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa SHUWASA, Afisa
Uhusiano wa Umma Nsianel Gerald, ameipongeza shule hiyo kwa mafanikio makubwa
na nidhamu ya wanafunzi na walimu.
Amesema, SHUWASA itaendelea kushirikiana na shule
katika kutatua changamoto zilizopo, ikiwemo kusaidia maboresho ya miundombinu
na mazingira ya kufundishia.
“Sisi kama SHUWASA tutawawekea madirisha
ya Vioo, Meza na viti vyake”amesema Nsianel
Wahitimu wakiwasili kwa ajili ya kuanza sherehe yao.
Wahitimu wakiwasili kwa ajili ya kuanza sherehe yao.
Mkuu wa shule ya msingi Lubaga Mwalimu Stella Lucas Halimoja, akizungumza kwenye mahafali ya 17 leo Septemba 19, 2025.

Mkuu wa shule ya msingi Lubaga Mwalimu Stella Lucas Halimoja, akizungumza kwenye mahafali ya 17 leo Septemba 19, 2025.

Mkuu wa shule ya msingi Lubaga Mwalimu Stella Lucas
Halimoja, akizungumza kwenye mahafali ya 17 leo Septemba 19, 2025.







Mgeni rasmi ,Nsianel Gerald akikabidhi Zawadi kwa wanafunzi ambaye ameimba wimbo wenye ujumbe kwa wahitimu.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald akizungumza kwenye mahafali
hayo ya shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald akizungumza kwenye mahafali
hayo ya shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald akizungumza kwenye mahafali
hayo ya shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na
Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la
kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambaye amewakilishwa na Afisa Uhusiano wa Umma wa SHUWASA,Nsianel Gerald, akiendelea na zoezi la kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa shule ya msingi Lubaga leo Septemba 19, 2025.







🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment