Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwanaume mmoja aliyefahamika
kwa jina la Juma Mpuya mwenye umri wa Miaka 45, mlinzi wa maduka ya mfanyabiashara amekutwa ameuawa na watu wasiojulikana katika eneo lake la kazi Mjini
Shinyanga.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Septemba
17, 2025, katika mtaa wa Majengo Mapya, kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.
Kwa mujibu wa mashuhuda, mwili
wa marehemu ulikutwa umefungwa sehemu za mikono na miguu na kuwekwa chini, huku
baadhi ya mali zilizokuwa dukani zikidaiwa kuibiwa.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa
mtaa wa Majengo Mapya, Bwana. Philimon Chikala, ameeleza kupokea taarifa za
tukio hilo kutoka kwa wananchi na kufika eneo la tukio kwa ajili ya hatua za
awali.
Akizungumza na Misalaba Media, Kamanda
wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,
Janeth Magomi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa jeshi la
polisi limeanza uchunguzi wa kina.
“Ni kweli tukio
hili limetokea, na tunashikilia mtuhumiwa mmoja kwa mahojiano. Jeshi la polisi
linaendelea na uchunguzi kuhakikisha wahusika wote wanakamatwa na kufikishwa
kwenye vyombo vya sheria,” amesema Kamanda
Magomi.
Jeshi la Polisi limewahimiza wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kufanikisha kukamatwa kwa wahalifu na kuimarisha usalama katika mkoa huo.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment