" MAHAFALI YA 16 SEKONDARI NDALA: WAHITIMU 2025 WAJIPANGA KULIANDIKIA TAIFA HISTORIA YA UFAULU

MAHAFALI YA 16 SEKONDARI NDALA: WAHITIMU 2025 WAJIPANGA KULIANDIKIA TAIFA HISTORIA YA UFAULU

WAHITIMU WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2025  SHULE YA SEKONDARI NDALA WAKISHEREHEKEA MAHAFARI YA 16 YA KIDATO CHA NNE TANGU KUANZA KWA SHULE HIYO

NA MWANDISHI WETU SHINYANGA

Wahitimu kidato cha nne mwaka 2025 Shule ya Sekondari Ndala, Manispaa ya Shinyanga, wameahidi kufanya vizuri katika Mtihani wa Taifa unaotarajiwa kuanza Novemba 10, 2025.

Ahadi hiyo wameitoa leo Septemba 18, 2025 katika mahafali ya 16 ya kidato cha nne, ambapo walibainisha kuwa mazingira bora ya kujifunzia na juhudi kubwa za walimu wao yamewajenga ipasavyo kufanikisha ndoto zao za kitaaluma na maisha ya baadaye.

Mkuu wa shule hiyo, Mwl. Hamisa Boniphace, aliwashukuru walimu kwa kujitolea na wazazi kwa mshirikiano wao wa karibu, akisema mshikamano huo ndio chachu ya mafanikio ya wanafunzi hao.

MKUU WA SHULE YA NDALA MWL. HAMISA BONIPHACE AKISOMA RISALA KWENYE MAHAFARI YA 16 YA KIDATO CHA NNE 2025 KWA MGENI RASMI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NDALA MANISPAA YA SHINYANGA.

Kwa upande wake, Mwl. Richard Makoye, aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, aliwasihi wazazi kuendelea kuwapa wanafunzi muda na mazingira tulivu ya kujisomea ili kuwawezesha kufanikisha malengo yao ya kitaaluma.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mhe. Magreth Baraka Ezekiel – Mwenyekiti wa Wachimbaji wa Madini Vijana Tanzania na Mkurugenzi wa Africa Mining Investment Fund – aliwahimiza wanafunzi hao kuendelea kuzingatia elimu kama msingi wa mafanikio ya mtu binafsi na maendeleo ya taifa.

“Elimu ndiyo dira ya maisha na msingi wa taifa imara. Endeleeni kuwa na nidhamu, juhudi na kujituma ili muwe chachu ya maendeleo kwa taifa la kesho,” alisema Mhe. Magreth.

 

Shule ya Sekondari Ndala imekuwa mfano wa kuigwa kutokana na mwelekeo chanya wa ufaulu wa wanafunzi wake. Mwaka 2024, shule hiyo ilishika nafasi ya 3 kati ya shule 21 za serikali katika Manispaa ya Shinyanga kwa kupata asilimia 95 ya ufaulu, ikilinganishwa na asilimia 90 mwaka 2023.

Mafanikio haya yametoa matumaini makubwa kwamba wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2025 wataendeleza mwendelezo wa kung’ara kitaaluma na kuliandikia taifa historia mpya ya ufaulu.

 


🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA


 

Post a Comment

Previous Post Next Post