Akizungumza
kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Katibu Tawala Msaidizi
anayesimamia masuala ya elimu na mafunzo ya ufundi, Samson Hango, amesema
mtihani huo unatarajiwa kufanyika katika halmashauri zote sita za mkoa huo
ambazo ni Kahama Mjini, Kishapu, Msalala, Shinyanga Manispaa, Ushetu na
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Amesema
mkoa una jumla ya shule 664 zenye watahiniwa wa darasa la saba, ambapo kati ya
hizo shule 598 ni za serikali na shule 66 ni zisizo za serikali.
Hango amebainisha kuwa jumla ya watahiniwa ni 41,463, wakiwemo wavulana 17,525
na wasichana 23,938, ambapo asilimia 94.53 wanatoka katika shule za serikali na
asilimia 5.47 katika shule zisizo za serikali.
"Hadi
kufika leo maandalizi yote yamekamilika, hakuna changamoto yoyote
iliyojitokeza. Tunategemea mtihani uende vizuri kwa siku zote mbili," amesema Hango.
Misalaba
Media imezungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule za manispaa ya Shinyanga,
ikiwemo Shule ya Msingi Mwenge, wamesema wako tayari kwa ajili ya mtihani huo
kutokana na maandalizi mazuri waliyoyafanya.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Mwenge, Esther Mbai ameeleza kuwa walimu wamefanya maandalizi ya
kutosha kuhakikisha wanafunzi wao wanafanya vizuri kwenye mtihani huo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia masuala ya elimu na mafunzo ya ufundi, Samson Hango, akizungumza na waandishi wa habari.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment