" MBUNGE MSTAAFU WA VITI MAALUM SALOME MAKAMBA ATIMIZA HAKI YA KIKATIBA KWA KUPIGA KURA

MBUNGE MSTAAFU WA VITI MAALUM SALOME MAKAMBA ATIMIZA HAKI YA KIKATIBA KWA KUPIGA KURA

Mbunge wa Viti Maalum mstaafu kutoka Mkoa wa Shinyanga, Salome Makamba, leo Oktoba 29, 2025, mapema asubuhi ametimiza haki yake ya kikatiba kwa kupiga kura kuchagua viongozi katika nafasi ya Udiwani, Ubunge na Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Makamba amepiga kura katika Kituo cha Kupigia Kura Bugweto, kilichopo Shule ya Msingi Bugweto, Kata ya Ibadakuli, ndani ya Jimbo la Shinyanga Mjini.

Akizungumza na Misalaba Media baada ya kupiga kura, amesema amefurahishwa na utulivu uliopo katika kituo hicho na amewahimiza wananchi wote waliojiandikisha kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya msingi kwa amani na utulivu.

Amesema kuwa zoezi la kupiga kura ni msingi wa demokrasia, hivyo ni muhimu kila mwananchi kushiriki ili kuchagua viongozi wanaoamini watawaletea maendeleo.


 


Post a Comment

Previous Post Next Post