
Raia wa Ghana Frederick Kumi maarufu mtandoni ‘Abu Trica’ amekamatwa kwa tuhuma za utapeli wa kimapenzi na kuwaibia wazee na watu wazima ambao ni Wazungu nchini Marekani kiasi cha fedha Dola milioni 8 za Marekani.
Waendesha mashtaka wa Marekani wanasema kijana huyo mwenye miaka 31, alitumia zana za akili bandia (AI) kuunda utambulisho usio wa kweli, pia aliwasiliana na waathiriwa kupitia tovuti za kutafuta wapenzi na mitandao ya kijamii, kisha polepole akajenga imani yao kabla ya kuwaomba fedha.
Abu Trica anakabiliwa na mashtaka nchini Marekani ya kula njama ya kufanya udanganyifu wa kielektroniki (wire fraud) na utakatishaji wa fedha na akipatikana na hatia, anaweza kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka 20 jela.
Wachunguzi wanasema Abu Trica, ambaye pia hutumia jina jingine Emmanuel Kojo Baah Obeng, amekuwa akiwasiliana na kina mama hao watu wazima kupitia simu, baruapepe na ujumbe wa maandishi.
Inadaiwa mbinu ambayo hutumia kuwapata huanza kwa kuwaeleza taarifa za kusikitisha zinazomhusu za kiafya, matatizo ya safari au fursa za biashara akiwa na lengo kuwashawishi kutuma fedha au vitu vya thamani.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment