" KUANZISHWA KWA MASHINDANO YA “COCOA CUP” – WILAYA YA MISSENYI, MKOA WA KAGERA

KUANZISHWA KWA MASHINDANO YA “COCOA CUP” – WILAYA YA MISSENYI, MKOA WA KAGERA

Na Lydia Lugakila -Misalaba media

Missenyi 

Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera inatarajiwa kuandika historia mpya baada ya kutangazwa rasmi kuanzishwa kwa Mashindano ya “Cocoa Cup”, yatakayofanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2026, yakishirikisha kata zote 20 za wilaya hiyo.

Mashindano hayo yanaratibiwa na Jonathan Jesse, yakilenga kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu kilimo cha Cocoa (Kakao) kama zao la kimkakati na lenye faida kubwa kiuchumi.

Dhamira ya Mashindano

Lengo kuu la Cocoa Cup ni kutangaza fursa za kilimo cha Cocoa kwa vitendo, kwa kutumia michezo, sanaa na utamaduni kama nyenzo ya kujenga uelewa, hamasa na motisha kwa wananchi wa Missenyi, hususan vijana na wanawake, ili wachangamkie kilimo hicho chenye tija.

Kwa mujibu wa Jesse Kata zitakazoshiriki

Mashindano ni kata zote 20 za Wilaya ya Missenyi ambazo ni: Bugandika, Bugorora, Buyango, Bwanjai, Gera, Ishozi, Ishinju, Kakunyu, Kanyigo, Kashenye, Kassambya, Kilimilile, Kitobo, Kyaka, Mabale, Minziro, Mushasha, Mutukula, Nsunga na Ruzinga.

Michezo na shughuli Zitakazoshindaniwa

Mashindano ya Cocoa Cup yatahusisha wanaume na wanawake katika michezo na shughuli zifuatazo:

mpira wa miguu

Ngoma za asili

Riadha (mbio za kukimbia)

Kuruka kamba / Kuguruka

Bao la asili (Olweso)

Matokeo yanayotarajiwa

Kupitia mashindano haya, Wilaya ya Missenyi inalenga

Kuongeza uelewa wa Wananchi kuhusu kilimo cha Cocoa,

Kuchochea ushiriki wa jamii katika kilimo cha kisasa

Kukuza vipaji vya michezo na utamaduni,

Kujenga mshikamano na umoja miongoni mwa kata za wilaya.

Mashindano ya Cocoa Cup yanatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku yakiiweka Missenyi katika ramani ya uzalishaji wa Cocoa nchini.

Post a Comment

Previous Post Next Post