" MSHAGATILA AAPISHWA RASMI DIWANI WA KATA YA KOLANDOTO: MWANZO MPYA WA MAENDELEO KATA YA KOLANDOTO

MSHAGATILA AAPISHWA RASMI DIWANI WA KATA YA KOLANDOTO: MWANZO MPYA WA MAENDELEO KATA YA KOLANDOTO

Na Elias Gamaya -SHINYANGA

Diwani mpya wa Kata ya Kolandoto katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Mshagatila Moses Kashinje, ameapishwa rasmi leo Desemba 04, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwl. Alexius Kagunze, Manispaa ya Shinyanga.

 Akizungumza mara baada ya kuapishwa, Mhe. Mshagatila ameahidi kushirikiana kwa karibu na wananchi, viongozi wa mitaa pamoja na watumishi wa Halmashauri katika kutatua changamoto zinazoikabili Kolandoto, akisisitiza kuwa maendeleo ya wananchi ndiyo kipaumbele chake kikuu.

 Kuapishwa kwa Mhe. Mshagatila kunafungua ukurasa mpya wa uongozi katika kata hiyo, ambapo wananchi wanatarajia kuona kasi mpya ya maendeleo, uwajibikaji ulio imara na utatuzi wa changamoto zinazowakabili katika maisha yao ya kila siku.









 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post