WABABE wawili wanatarajiwa kukutana uwanjani kwenye msako wa bingwa mpya wa NMB Mapinduzi Cup, Januari 13,2026.
Ni Azam FC vs Yanga SC hawa watakuwa na kazi kufika hitimisho la mashindano haya ambayo yalikuwa na ushindani mkubwa katika hatua za makundi, nusu fainali na sasa fainali.
Yanga SC iliwaondoa Singida Black Stars na Azam FC iliwaonoda Simba SC kwenye hatua ya nusu fainali na timu zote zilipata ushindi wa goli 1-0 katika hatua hiyo.
Timu zote zimeanza maandalizi tayari kwa mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya uwanja ambao utatoa maamuzi nani atakuwa bingwa.
Goli la Azam FC dhidi ya Simba SC lilifungwa na Lameck Lawi ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora na lile la Yanga SC vs SBS lilifungwa na Maxi Nzengeli.
Ni mbinu za Florent Ibenge Kocha Mkuu wa Azam FC vs mbinu za Pedro Goncalves, Kocha Mkuu wa Yanga SC zitakuwa kazini msako wa taji.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment