Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Ndg.
Jimotoli Jilala Maduka, tarehe 10 Januari 2026, ameongoza kikao kazi cha
dharura kilichowakutanisha makatibu wa kata wa Jumuiya ya Wazazi CCM wilayani
humo kwa lengo la kutoa maelekezo ya utekelezaji wa majukumu yao kwa mwaka
2026.
Katika kikao hicho, Ndg.
Maduka amewahimiza makatibu wa kata kuongeza ufanisi, bidii na juhudi katika
kazi za Jumuiya pamoja na kuimarisha mshikamano na umoja ndani ya chama,
akisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa ushirikiano ili kukiimarisha chama
katika ngazi zote.
Aidha, amesisitiza
umuhimu wa kuendelea kusajili wanachama wapya wengi zaidi, kutoa hamasa kwa
wanachama kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama pamoja na kulipa ada
kwa hiari kama sehemu ya kukijenga chama kiuchumi na kiutendaji.
Ndg. Maduka ameelekeza
makatibu wote wa kata kwenda chini kwa wananchi kuhamasisha utekelezaji wa
majukumu ya Jumuiya kwa mwaka 2026, huku akiwataka wajumbe na wanachama
kutambua wajibu wao na kuutekeleza ipasavyo kwa maendeleo ya Jumuiya na chama
kwa ujumla.
Katika hatua nyingine,
Katibu huyo ameagiza kila kata kubuni miradi mbalimbali ya kiuchumi ya Jumuiya
ya Wazazi CCM kwa lengo la kuongeza kipato na kuchochea maendeleo ya kiuchumi
ndani ya Jumuiya hiyo wilayani Mpanda.
Akihitimisha kikao kazi
hicho cha kwanza kwa mwaka 2026, Ndg. Jimotoli Jilala Maduka amewapongeza
makatibu kwa mahudhurio mazuri, anawahamasisha kuendelea kufanya kazi kwa
bidii, uadilifu na kuzingatia misingi ya uongozi bora ili kuleta tija katika Jumuiya
na Chama cha Mapinduzi.
Kwa pamoja, wajumbe wa kikao wamekubaliana kuyatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa kwa lengo la kuimarisha Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda na kuchangia maendeleo ya chama na jamii kwa ujumla.


🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment