Na Mapuli Kitina Misalaba
Shirika la Companion of Women and Children Empowerment
(COWOCE) limefanya mafunzo maalum kwa vikundi vya VICOBA leo tarehe 17 Januari
2026 katika Manispaa ya Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kuinua
uchumi wa wananchi na kuwawezesha kiuchumi.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Shirika la COWOCE
yakilenga kuwajengea uwezo wanachama wa VICOBA katika uendeshaji wa vikundi
vyao, usimamizi wa fedha na matumizi sahihi ya mikopo kwa ajili ya shughuli za
kiuchumi ambapo mafunzo hayo yamehudhuriwa na wanachama kutoka vikundi
mbalimbali vya VICOBA vilivyopo Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi
wa Shirika la COWOCE, Bwana Joseph Ndatala, amesema lengo kuu la shirika hilo
ni kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapa elimu sahihi itakayowasaidia kujitegemea
na kuboresha maisha yao ya kila siku.
Kwa upande wake, Meneja wa Shirika la COWOCE, Veronica
Kipangule, ameeleza kuwa shirika hilo limejikita katika kusaidia makundi
mbalimbali hususan wanawake na vijana kupitia mafunzo ya ujasiriamali, VICOBA
pamoja na miradi midogo midogo ya kiuchumi yenye tija kwa familia na jamii kwa
ujumla.
Mada ya kwanza imewasilishwa na Mkufunzi wa COWOCE
Bwana Joseph Ndatala, ikilenga kuwajengea wanachama uelewa wa dhana ya VICOBA,
umuhimu wake na namna ya kuendesha kikundi kwa ufanisi.
Katika mada hiyo, washiriki wamejifunza maana ya
VICOBA, malengo na faida zake, kanuni na taratibu za uendeshaji, muundo wa
kikundi pamoja na haki na wajibu wa mwanachama. Mafunzo hayo yanatolewa kwa
njia ya majadiliano ya pamoja, maswali na majibu pamoja na mifano halisi kutoka
katika vikundi vya washiriki.
Imeelezwa kuwa VICOBA ni vikundi vya watu
wanaojikusanya kwa hiari ili kuweka akiba, kukopeshana fedha na kusaidiana
kiuchumi, huku malengo yake yakiwa ni kukuza tabia ya kujiwekea akiba, kutoa
mikopo midogo kwa wanachama, kuimarisha umoja na mshikamano na kuinua kipato
cha familia na jamii.
Ndatala ametaja faida za VICOBA kuwa ni urahisi wa
kujiunga na kuendesha, kutokuwa na masharti magumu kama ya benki, kutoa mikopo
kwa wakati pamoja na kujenga nidhamu ya kifedha kwa wanachama.
Washiriki pia wamejifunza muundo wa VICOBA
unaojumuisha Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina na wajumbe wa kamati, ambapo kila
kiongozi anawajibika kusimamia kikundi kwa uaminifu na uwazi.
Mada ya pili imelenga kuwajengea wanachama uwezo wa
kusimamia fedha za kikundi na mikopo kwa uwazi na nidhamu ambapo washiriki wamefundishwa
kuhusu akiba na michango ya wanachama, utunzaji wa fedha kwa kutumia sanduku
lenye funguo tatu au benki, pamoja na umuhimu wa kumbukumbu sahihi za mapato na
matumizi.
Aidha, masharti ya mikopo, riba na marejesho
yameelezewa kwa kina, huku mkazo mkubwa ukiwekwa kwenye athari za mikopo
chechefu ambayo husababisha kukosekana kwa fedha kwenye kikundi, migogoro
miongoni mwa wanachama na kudhoofika kwa VICOBA.
Katika mada hiyo, washiriki wanafanya mazoezi ya
vitendo ikiwemo hesabu rahisi za mkopo, mfano wa mkopo wa shilingi 300,000 kwa
riba ya asilimia 15, ili kuwajengea uelewa wa vitendo kuhusu marejesho.
Mada ya tatu imelenga kuwasaidia wanachama kutumia
mikopo ya VICOBA katika shughuli za kiuchumi zitakazowaongezea kipato.
Washiriki wanafundishwa maana ya ujasiriamali, sifa za mjasiriamali bora,
uchaguzi wa biashara ndogo, matumizi sahihi ya mkopo pamoja na namna ya
kutenganisha fedha za biashara na matumizi ya nyumbani.
Imeelezwa kuwa ujasiriamali ni uwezo wa kuona fursa,
kuanzisha au kuboresha shughuli za kiuchumi na kuchukua hatua kwa ujasiri ili
kupata faida na kuboresha maisha. Washiriki wanahimizwa kutumia mikopo kwa
biashara zenye soko, kuendana na mazingira yao na kuanza kwa mtaji mdogo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwemo akina
mama wanufaika wa miradi ya Shirika la COWOCE, wameeleza kuridhishwa na mafunzo
hayo wakisema yamewapa uelewa mpana juu ya uendeshaji sahihi wa VICOBA,
usimamizi wa fedha na matumizi bora ya mikopo.
Wanufaika hao wanaeleza kuwa kabla ya mafunzo walikuwa
wakikumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo mikopo chechefu, migogoro ndani ya
vikundi pamoja na matumizi yasiyo sahihi ya fedha za mikopo.
Akina mama hao wameeleza kuwa elimu waliyoipata
itawasaidia kuimarisha vikundi vyao, kuongeza nidhamu ya kifedha, kukuza
biashara ndogo ndogo wanazozifanya pamoja na kuboresha maisha ya familia zao
huku akilishukuru shirika la COWOCE kwa kuendelea kuwa karibu na jamii kwa
vitendo kupitia mafunzo, miradi ya kiuchumi na misaada ya kijamii ikiwemo elimu
na mradi wa nguruwe unaolenga ustawi wa watoto.
Wanufaika hao wameahidi kutumia maarifa waliyoyapata
kuleta mabadiliko chanya katika vikundi vyao na kuwa mabalozi wa VICOBA bora
katika jamii zao, huku wakiiomba COWOCE kuendelea kutoa mafunzo ya mara kwa
mara ili kuwafikia wananchi wengi zaidi wa Mkoa wa Shinyanga.
Katika hatua nyingine, Shirika la COWOCE limekabidhi
msaada wa madaftari kwa wanafunzi wa shule za msingi zilizopo Kata ya Ndala,
ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika kuboresha mazingira ya elimu.
Vilevile, shirika hilo lina utaratibu wa utekelezaji wa mradi wa nguruwe, ambapo hugawa nguruwe wawili kwa kila familia, nguruwe hao wakilenga kusaidia mahitaji ya watoto ikiwemo kugharamia masomo yao, hatua inayolenga kusaidia watoto kutimiza ndoto zao za kielimu.
Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwana Joseph Ndatala, akizungumza na washiriki wakati wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika leo tarehe 17 Januari 2026 mjini Shinyanga.


Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwana Joseph Ndatala,
akizungumza na washiriki wakati wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika leo tarehe
17 Januari 2026 mjini Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwana Joseph Ndatala,
akizungumza na washiriki wakati wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika leo tarehe
17 Januari 2026 mjini Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwana Joseph Ndatala,
akizungumza na washiriki wakati wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika leo tarehe
17 Januari 2026 mjini Shinyanga.

Mshiriki wa mafunzo ya VICOBA akiuliza maswali na
kuchangia hoja wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la COWOCE ambayo
yamefanyika leo mjini Shinyanga.

Mshiriki wa mafunzo ya VICOBA akiuliza maswali na
kuchangia hoja wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la COWOCE ambayo
yamefanyika leo mjini Shinyanga.

Mshiriki wa mafunzo ya VICOBA akiuliza maswali na
kuchangia hoja wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la COWOCE ambayo
yamefanyika leo mjini Shinyanga.

Meneja wa Shirika la COWOCE, Veronica Kipangule, akieleza malengo ya shirika hilo
kwa washiriki wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika mjini Shinyanga leo Januri 17,
2026.

Meneja wa Shirika la COWOCE, Veronica Kipangule, akieleza malengo ya shirika hilo
kwa washiriki wa mafunzo ya VICOBA yaliyofanyika mjini Shinyanga leo Januri 17,
2026.

Mshiriki wa mafunzo ya VICOBA akiuliza maswali na
kuchangia hoja wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la COWOCE ambayo
yamefanyika leo mjini Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwwana Joseph
Ndatala, akikabidhi madaftari kwa wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya
Ndala Manispaa ya Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwwana Joseph
Ndatala, akikabidhi madaftari kwa wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya
Ndala Manispaa ya Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwwana Joseph
Ndatala, akikabidhi madaftari kwa wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya
Ndala Manispaa ya Shinyanga.

Mkurugenzi wa Shirika la COWOCE, Bwwana Joseph
Ndatala, akikabidhi madaftari kwa wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya
Ndala Manispaa ya Shinyanga.


Washiriki wa mafunzo ya VICOBA, pamoja na Mkurugenzi Bwana Joseph Ndatala na Meneja Veronica Kipangule wa Shirika la COWOCE, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanikisha mafunzo hayo leo tarehe 17 Januari 2026.























Post a Comment