Na: Belnardo Costantine, Misalaba Media- Uganda.
Tume ya Uchaguzi imemtangaza Mwanasiasa Mkongwe na Jeneraki wa zamani wa jeshi la Uganda.Yoweri Kaguta Museveni, mwenye umri wa Miaka 81, kuwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Uganda uliofanyika Januari 15, 2026, akipata Asilimia 71.6 ya jumla ya kura halali zilizopigwa, na kuendeleza utawala wake zaidi ya miongo minne na kuwashinda wapinzani wake Kwa kishindo kikubwa cha kiasi cha kura zilizopigwa na Wananchi wa Uganda na kumpa ushindi wa kishindo.
Hata hivyo, chama cha Bobi Wine kimehoji uhalali wa matokeo hayo, kikidai kuwa kiongozi huyo wa upinzani alichukuliwa kwa nguvu kutoka nyumbani kwake jijini Kampala,Madai ambayo yamepingwa na mamlaka ya nchini hapa msemaji wa polisi alisema hawana taarifa hiyo.
Aidha mamlaka ya mawasiliano nchini hapa "UCCA' ilizima mtandao wa internet Kwa lengo la kudhibiti udanganyifu na taarifa potofu wakati wa uchaguzi.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


Post a Comment