" CDF MKUNDA AFUNGA MAFUNZO YA KIJESHI ,AWAPA NENO ASKARI WAPYA.

CDF MKUNDA AFUNGA MAFUNZO YA KIJESHI ,AWAPA NENO ASKARI WAPYA.


 Na: Belnardo Costantine, Misalaba Media


‎Mku wa Jeshi la  wananchi wa Tanzania (JWTZ)Jenerali Jacob John Mkunda amefunga rasmi mafunzo ya askari wapya katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi "RTS" Kihangaiko Msata mkoani Pwani.

‎Aidha Jenerali Mkunda amewataka askari wapya kukiishi na kuzingatia kiapo cha utii wakati wote watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao sehemu mbalimbali watakayopangiwa, huku akisisitiza kuchukuliwa hatua kwa askari watakaokwenda kinyume na kiapo chao.

‎Askari hao  wameaswa kuendelea kukiishi kiapo cha kijeshi kitakacho waweka mbali na  mambo ambayo ni kinyume na taratibu za kijeshi ikiwemo kutojihusisha na siasa, matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, matumizi ya dawa za kulevya, michezo ya kamari na kuepuka madeni yasiyo na tija.

‎Hatahivyo Mkuu wa Majeshi amewataka askari hao kutunza afya zao na kuzingatia lishe bora wakati wote wanapotekeleza majukumu yao.




Post a Comment

Previous Post Next Post