Na: Mervat Sakr Imeidhihirisha Timu ya Taifa ya Misri ya mpira wa mkono ubabe wake kwenye jukwaa la kutwaa mataji ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya Mpira wa Mkono, lililofanyika nchini Rwanda, baada ya kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika mashindano yaliyotamatishwa kwa kutwaa taji la bara.Ushindi wa timu ya Misri ulipatikana baada ya kuifunga Timu ya Taifa ya Tunisia katika mchezo wa fainali, hatua iliyowawezesha “Mafarao” kutwaa taji lao la kumi la Afrika katika historia yao, na hivyo kuifikia rekodi ya Tunisia kama timu yenye mataji mengi zaidi ya bara.Timu ya Misri inaendelea kuthibitisha utawala wake katika ulingo wa Afrika, ambapo haijapoteza mchezo wowote wa mashindano ya bara tangu mwaka 2018. Katika toleo la sasa, Misri iliwasilisha kiwango cha juu na uthabiti mkubwa, na kuwa timu pekee iliyoshinda mechi zote za mashindano hayo, ikifika fainali kwa rekodi kamili, jambo linalothibitisha nguvu na ubora wake wa kiufundi.Katika hatua ya makundi, Mafarao waliongoza kundi lao baada ya kuibuka na ushindi katika mechi tatu mfululizo dhidi ya Gabon, Angola na Uganda, kabla ya kuendeleza mwendelezo wao mzuri katika hatua ya pili, wakiongoza kundi lao tena kwa ushindi dhidi ya Algeria, kisha kuipiga Nigeria kwa ushindi mnono.Katika nusu fainali, timu ya Misri ilifanikiwa kuondoa Cape Verde kwa ushindi wa 32–26, katika mchezo mkali uliotawaliwa na uzoefu mkubwa na uwezo wa hali ya juu wa wachezaji wa Misri.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment