Na Mapuli Kitina Misalaba
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana,
Mhe. Joel Nanauka amezindua rasmi Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga, hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
serikali, taasisi binafsi pamoja na vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa
wa Shinyanga, waliokusanyika kwa lengo la kushuhudia hatua hiyo inayolenga
kuimarisha ushiriki wa vijana katika maendeleo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Nanauka
amesema kupitia jukwaa hilo, Wizara itaimarisha mahusiano ya moja kwa moja kati
ya Serikali na vijana, pamoja na kutoa taarifa sahihi kuhusu mikopo na mitaji
inayotolewa kupitia mifuko ya serikali, programu wezeshi na taasisi za fedha.
Amesema lengo ni kuhakikisha vijana wanapata taarifa
kwa wakati na wanachangamkia fursa zilizopo bila ya kuzunguka huku na kule.
“Tunataka katika miaka mitano ya Rais Samia, vijana
wasihangaike kutafuta fursa, bali wao waamue wanataka fursa gani ili kuinua
uchumi wao,” amesema.
Waziri Nanauka amesisitiza kuwa jukwaa hilo ni sehemu
ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana iliyorejewa na
kuboreshwa mwaka 2024, inayolenga kuhakikisha vijana wanashiriki kikamilifu
katika maamuzi, wanapata ajira na fursa za ujasiliamali, wanakuwa wazalendo,
wabunifu na kizazi chenye maadili.
Ameongeza kuwa jukwaa hilo linaendana na maono ya Dira
ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kujenga Tanzania yenye uchumi
shindani, unaojitegemea na unaotegemea viwanda, teknolojia na rasilimali watu
wenye ujuzi.
“Ili kufikia lengo hilo vijana lazima wawe kitovu cha
uzalishaji, wawe kitovu cha ubunifu na pia wawe sehemu ya uongozi wa taifa
letu,” amesema.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni
Mhita amesema Mkoa umeendelea kuimarisha mazingira rafiki ya ujasiliamali kwa
kusimamia miongozo na sera jumuishi zinazowawezesha vijana kushiriki katika
shughuli za kiuchumi.
Amesema hadi sasa jumla ya wafanyabiashara 2,453
wamesajiliwa kupitia juhudi za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa katika kuratibu na
kusimamia zoezi la usajili wa wajasiliamali.
RC Mhita amewahimiza vijana kutumia ipasavyo fursa
zinazotolewa na Serikali, hususan wale wenye vipaji katika sekta mbalimbali.
Amesema si kila mtu ana kipaji, hivyo wenye vipaji
wanapaswa kuvitambua na kuviendeleza kwa kufuata taratibu za usajili kupitia
maafisa maendeleo na maafisa maendeleo ya vijana waliopo katika halmashauri.
Baadhi ya vijana waliohudhuria uzinduzi huo wameahidi
kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ili kujikwamua kiuchumi na
kuchangia maendeleo ya Mkoa wa Shinyanga.
Katika jukwaa hilo, mada na mijadala mbalimbali imewasilishwa, ambapo vijana wamejadili masuala ya ajira, ujasiliamali, mitaji, pamoja na namna ya kutumia teknolojia kama nyenzo ya kukuza uchumi wao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana,
Mhe. Joel Nanauka akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa
Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana,
Mhe. Joel Nanauka akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa
Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Dkt.
Kedmon Mapana akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga
leo Jumamosi Febuari 21, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza
kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21,
2026.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza
kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21,
2026.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro akizungumza
kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Febuari 21,
2026.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.
Vijana kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi wa Jukwaa la Vijana leo Februari 21, 2026 katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa ya Shinyanga.🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254























Post a Comment