" MAKATIBU WA JUMUIYA YA WAZAZI CCM MPANDA WATAKIWA KUIMARISHA UHAI NA MIRADI

MAKATIBU WA JUMUIYA YA WAZAZI CCM MPANDA WATAKIWA KUIMARISHA UHAI NA MIRADI



Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, akifungua kikao.

Makatibu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi ngazi ya kata wilayani Mpanda wametakiwa kuongeza juhudi katika kusimamia uhai wa jumuiya, kuibua miradi ya maendeleo na kuimarisha utendaji wao.

Wito huo umetolewa Machi 30, 2026 na Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Jimotoli Jilala Maduka, wakati akifungua kikao cha kawaida cha makatibu hao kilichoanza saa 4:00 asubuhi.

Akizungumza katika kikao hicho, Maduka aliwataka makatibu kuwa watulivu na makini katika kujadili ajenda mbalimbali, huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano katika kufanikisha majukumu ya jumuiya.

Katika tathmini ya vikao na matukio ya mwaka 2025, wajumbe walieleza kuridhishwa na utekelezaji wa majukumu, wakibainisha kuwa hakukuwa na changamoto kubwa zilizojitokeza katika kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama.

Kuhusu uhai wa jumuiya, Maduka aliwahimiza makatibu kuendelea kuhamasisha wanachama kulipa ada na kuandikisha wanachama wapya katika ngazi za matawi, mashina na kata ili kuimarisha jumuiya hiyo.

Aidha, aliwataka viongozi hao kufanya vikao vya mara kwa mara vya kikanuni pamoja na kuhakikisha wanatunza kumbukumbu sahihi za vikao na taarifa za wanachama kwa ajili ya rejea.

Katika ajenda ya miradi, makatibu walielekezwa kuibua na kuendeleza miradi ya kiuchumi itakayoongeza mapato ya jumuiya. Pia walitakiwa kuhakikisha miradi iliyopo inafufuliwa na kuendelezwa kwa lengo la kuimarisha uchumi wa jumuiya hiyo.

Maduka alisisitiza umuhimu wa kuendeleza juhudi za kuiboresha shule ya sekondari na ufundi ya Milala iliyopo Kata ya Misunkumilo, akibainisha kuwa hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha eneo la shule linapimwa na kupata hati miliki, hatua itakayosaidia kuvutia uwekezaji.

Kikao hicho pia kilijadili maandalizi ya maadhimisho ya Wiki ya Wazazi yanayotarajiwa kufanyika Mei 7, 2026, ambapo makatibu walitakiwa kuweka mikakati madhubuti ya kufanikisha shughuli hiyo.

Sambamba na hilo, viongozi hao walihimizwa kuendeleza umoja, mshikamano, nidhamu na ushirikiano ili kuhakikisha jumuiya inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, makatibu waliagizwa kufanya ziara katika kata na matawi kwa lengo la kuhamasisha uandikishaji wa wanachama, ulipaji ada pamoja na kutoa elimu na mafunzo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali.

Kikao hicho kilihitimishwa saa 7:00 mchana, ambapo viongozi walishukuru kwa ushiriki na michango ya mawazo iliyolenga kuboresha utendaji wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, akiwa kwenye picha ya pamoja na makatibu wa Jumuiya ya Wazazi kata.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, akiwa kazini na kuonyesha ubora wake wa haiba katika utekelezaji wa majukumu yake ya ofisini.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Kashaulili, Ndg. Sigulu, akichangia agenda katika kikao cha makatibu wa Jumuiya ya Wazazi kata.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi kata ya Katumba, Ndg. Jastine, akiunga mkono jitihada za Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, huku akitoa maelekezo mbalimbali ya kazi wakati wa kikao hicho.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Mpanda, Ndg. Maziku, akichangia agenda katika kikao hicho.

 

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


Post a Comment

Previous Post Next Post