Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenyekiti wa Maafisa Usafirishaji Wilaya ya Shinyanga, Mohamed Juma, amesisitiza umuhimu wa kulinda amani, akieleza kuwa ni msingi mkubwa wa shughuli za kila siku hususan kwa vijana wanaojihusisha na kazi za usafirishaji kama bodaboda.
Akizungumza na Misalaba Media, Mohamed amesema kuwa
bila amani, vijana wengi hawawezi kufanya kazi zao za kujipatia kipato,
akitolea mfano wa waendesha bodaboda ambao hutegemea utulivu wa mazingira ili
kuendesha shughuli zao kwa uhuru na usalama.
“Amani ni suala la msingi kuliko kitu chochote, kwa
sababu kama hakuna amani huwezi kutoka kwenda kuendesha bodaboda,” amesema.
Ameongeza kuwa katika tukio la maandamano
yaliyotarajiwa kufanyika tarehe 29 mkoani Shinyanga, hakukutokea vurugu yoyote
kutokana na msimamo wa vijana waliokataa kushiriki vitendo vinavyoweza
kuhatarisha usalama.
Amesema walikubaliana kwa pamoja kutoruhusu kupotoshwa
na baadhi ya wanasiasa au watu wachache wenye nia ya kuvuruga amani,
akibainisha kuwa hawako tayari kujiingiza kwenye migogoro kwa maslahi ya
wengine.
“Hatuko tayari kudanganywa na wanasiasa au
wahuni wachache ili sisi tuumie, wakati wao wanaendelea na maisha yao,”
ameongeza.
Mohamed ametoa rai kwa vijana kuendelea kuwa walinzi
wa amani, kuepuka kushawishika na fedha au ahadi zisizo na tija, na badala yake
kujikita katika shughuli halali za kujipatia kipato.
Amesisitiza kuwa kulinda amani ni jukumu la kila
mmoja, na kwamba jamii ikidumisha utulivu itaendelea kufungua fursa zaidi za
kiuchumi kwa vijana na taifa kwa ujumla.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment