
Mwalimu Richard Makoye (wa tatu kutoka kulia) akiongoza kikao cha tathmini ya matokeo ya mtihani wa pamoja kwa shule za sekondari za Manispaa ya Shinyanga, kilicholenga kuimarisha taaluma na ufaulu wa wanafunzi.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga,
Richard Makoye, leo Aprili 21, 2026 ameongoza kikao cha tathmini ya matokeo ya
mtihani wa pamoja wa mwezi Aprili, kilicholenga kuchambua maendeleo ya taaluma
na kuweka mikakati ya kuboresha ufaulu kwa wanafunzi wa shule za sekondari.
Kikao hicho kilihusisha jumla ya shule 31 za sekondari
kutoka Manispaa hiyo, huku washiriki 112 wakijumuisha Maafisa Elimu Kata, Wakuu
wa Shule, Makamu Wakuu wa Shule pamoja na walimu wa taaluma.
Akizungumza katika kikao hicho, Mwalimu Makoye amesema
tathmini hiyo ni sehemu ya juhudi za kuinua kiwango cha elimu kwa kubaini
changamoto zilizojitokeza katika matokeo ya mitihani na kuzipatia ufumbuzi wa
pamoja.
“Tunataka kuona mabadiliko chanya katika
matokeo ya wanafunzi, hivyo ni muhimu kwa walimu na viongozi wa elimu
kushirikiana kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati iliyowekwa,”
amesema Makoye.
Kwa upande wao, Maafisa Elimu Kata wakiongozwa na
mwenyekiti Aden Mwakatage pamoja na Grace Mwijarubi wamesisitiza umuhimu wa
ufuatiliaji wa karibu kwa walimu na wanafunzi ili kuhakikisha malengo ya
kitaaluma yanafikiwa.
Aidha, Mwenyekiti wa Wakuu wa Shule Mkoa, Kisandu
Seni, akishirikiana na Katibu Koletha Mgata, wamehimiza nidhamu ya kazi,
uwajibikaji pamoja na matumizi bora ya muda wa kujifunza.
Kikao hicho ni sehemu ya mkakati wa Manispaa ya Shinyanga kuimarisha taaluma na kuhakikisha wanafunzi wanapata matokeo bora zaidi katika mitihani yao.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




















Post a Comment