Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce
Mwizarubi, ameanza rasmi ziara ya kutembelea vyuo takribani 17 vilivyopo mkoani
humo, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uongozi wa wanafunzi, kusikiliza changamoto
zao pamoja na kuhamasisha matumizi bora ya fursa zinazotolewa na serikali.
Katika ziara hiyo, Mwizarubi ameambatana na Katibu wa
Seneti Mkoa wa Shinyanga Bwana Lukomanga Jinyage Jiboli, Katibu Hamasa wa
Seneti Sharon Callist Mathias pamoja na Mjumbe wa kamati ya uratibu Seneti Mkoa
wa Shinyanga Mercy Saimon Shauri ambapo wameanza kwa kutembelea vyuo mbalimbali ikiwemo Hill Forest
College na VETA Kishapu.
Akizungumza na wanachuo wa Hill Forest College,
Mwizarubi amewataka vijana kuthamini na kutumia kikamilifu fursa wanazopewa na
serikali, hususan katika kupata elimu na ujuzi unaowawezesha kujiajiri au
kupata ajira.
“Tuna kila sababu ya kumshukuru Mheshimiwa
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuridhia na kuidhinisha bajeti
zinazolenga kuwasaidia vijana. Niwaombe sana vijana wenzangu, hasa waliopata
fursa hizi, kuzitumia vizuri. Pia tuendelee kuunga mkono juhudi za serikali ya
awamu ya sita, na pale tunapokutana na changamoto, tuwasilishe kwa viongozi
wanaohusika,” amesema Mwizarubi.
Baadhi ya wanachuo wa Hill Forest College wanaonufaika
na ufadhili wa serikali wameishukuru serikali kwa kuwapatia fursa ya kusoma
bure, huku wakimpongeza Mwenyekiti wa Seneti kwa kuanzisha ziara hiyo ambayo
wamesema ina umuhimu mkubwa kwa maendeleo yao na wameomba iwe endelevu.
Aidha, katika ziara hiyo, viongozi hao wametembelea
pia Chuo cha VETA Kishapu, ambapo Mwizarubi amezungumzia mipango mbalimbali ya
Seneti ikiwemo kuandaliwa kwa semina kubwa itakayowakutanisha wanachuo wote wa
vyuo vya Mkoa wa Shinyanga ili kujadili fursa na changamoto zinazowakabili
vijana.
Ameongeza kuwa Seneti ya Mkoa pia inatarajia kuratibu
mahafali ya pamoja kwa wahitimu wa vyuo mbalimbali, hatua ambayo inalenga
kuimarisha mshikamano na kutoa heshima kwa wanafunzi wanaohitimu masomo yao.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo amesimamia
uchaguzi wa viongozi wapya wa Seneti katika baadhi ya vyuo vilivyotembelewa,
ambapo nafasi mbalimbali zikiwemo za mwenyekiti, katibu na viongozi wengine
zimejazwa. Pia amekabidhi vifaa vya kazi kwa viongozi hao, ikiwemo vitabu vya
kumbukumbu (counter books) na mafaili kwa ajili ya kuhifadhi taarifa za Seneti
katika kila chuo.
Kwa upande wao, baadhi ya wanafunzi wa VETA Kishapu
wamempongeza Mwizarubi kwa ziara hiyo, wakisema imeleta hamasa mpya kwa
wanafunzi, huku wakieleza kuwa utoaji wa zawadi na vifaa ni jambo jipya ambalo
halijawahi kufanywa tangu kuanzishwa kwa Seneti, na wameahidi kutoa ushirikiano
wa karibu kwa viongozi hao.
Leo, ziara hiyo imefanikiwa kutembelea vyuo viwili,
huku ikitarajiwa kuendelea katika vyuo vingine vya Mkoa wa Shinyanga katika
siku zijazo.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiongozwa na Mwenyekiti Jackson Aloyce Mwizarubi wakiwasili VETA Kishapu, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutembelea vyuo 17 mkoani humo.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiongozwa na Mwenyekiti Jackson Aloyce Mwizarubi wakiwasili VETA Kishapu, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutembelea vyuo 17 mkoani humo.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiongozwa na Mwenyekiti Jackson Aloyce Mwizarubi wakiwasili VETA Kishapu, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutembelea vyuo 17 mkoani humo.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akizungumza baada ya kuwasili VETA Kishapu.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akizungumza baada ya kuwasili VETA Kishapu.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage Jiboli akizungumza baada ya kuwasili VETA Kishapu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia baada ya kuwasili VETA Kishapu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia baada ya kuwasili VETA Kishapu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia baada ya kuwasili VETA Kishapu.

Mjumbe wa kamati ya uratibu Seneti Mkoa wa Shinyanga Mercy Saimon Shauri

Mjumbe wa kamati ya uratibu Seneti Mkoa wa Shinyanga Mercy Saimon Shauri

Mjumbe wa kamati ya uratibu Seneti Mkoa wa Shinyanga Mercy Saimon Shauri
akizungumza na wanachuo, akisisitiza umuhimu wa mshikamano na ushirikiano katika kuimarisha uongozi wa wanafunzi.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akihimiza wanachuo kushiriki kikamilifu katika shughuli za Seneti na kuchangamkia fursa zinazotolewa.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akihimiza wanachuo kushiriki kikamilifu katika shughuli za Seneti na kuchangamkia fursa zinazotolewa.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia fursa za mafunzo ya ufundi na umuhimu wa kujiajiri kwa vijana wa VETA Kishapu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia fursa za mafunzo ya ufundi na umuhimu wa kujiajiri kwa vijana wa VETA Kishapu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumzia fursa za mafunzo ya ufundi na umuhimu wa kujiajiri kwa vijana wa VETA Kishapu.
Rais wa Veta Kishapu ambaye pia ni Mwenyekiti mpya wa Seneti tawi la Kishapu Alphonce Nicholaus Edward akiwashukuru viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akiwa katika zoezi la kukabidhi kaunta book na mafaili kwa viongozi wa wanafunzi wa Seneti VETA Kishapu, kwa lengo la kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na ufanisi wa kazi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akiwa katika zoezi la kukabidhi kaunta book na mafaili kwa viongozi wa wanafunzi wa Seneti VETA Kishapu, kwa lengo la kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na ufanisi wa kazi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akiwa katika zoezi la kukabidhi kaunta book na mafaili kwa viongozi wa wanafunzi wa Seneti VETA Kishapu, kwa lengo la kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na ufanisi wa kazi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akihamasisha wanachuo wa Hill Forest kutumia vizuri fursa za elimu na kujiandaa kujiajiri.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akihamasisha ushiriki wa wanachuo katika shughuli za maendeleo na uongozi.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akihamasisha ushiriki wa wanachuo katika shughuli za maendeleo na uongozi.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon Callist Mathias akihamasisha ushiriki wa wanachuo katika shughuli za maendeleo na uongozi.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage Jiboli akieleza mipango ya Seneti katika kuimarisha uongozi wa wanafunzi chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akisimamia uchaguzi katika chuo cha Hill Forest Shinyanga.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akihamasisha wanachuo wa Hill Forest kutumia vizuri fursa za elimu na kujiandaa kujiajiri.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akihamasisha wanachuo wa Hill Forest kutumia vizuri fursa za elimu na kujiandaa kujiajiri.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akihamasisha wanachuo wa Hill Forest kutumia vizuri fursa za elimu na kujiandaa kujiajiri.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akiwa katika zoezi la kukabidhi kaunta book na mafaili kwa viongozi wa wanafunzi wa Chuo cha Hill Forest Shinyanga, kwa lengo la kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na ufanisi wa kazi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akiwa katika zoezi la kukabidhi kaunta book na mafaili kwa viongozi wa wanafunzi wa Chuo cha Hill Forest Shinyanga, kwa lengo la kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na ufanisi wa kazi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akihamasisha wanachuo wa Hill Forest kutumia vizuri fursa za elimu na kujiandaa kujiajiri.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254















































Post a Comment