Na Mapuli Kitina Misalaba
Wakristo
wamekumbushwa umuhimu wa kusoma na kuelewa maandiko matakatifu ya Biblia ili
kuepuka kupotoshwa na mafundisho ya manabii wa uongo yanayoendelea kujitokeza
katika jamii.
Wito huo umetolewa na Askofu Carlton Potts kutoka
Texas, Marekani, wakati akihubiri katika ibada ya Jumapili iliyofanyika leo
Aprili 12, 2026 Kanisa la AICT Kambarage, mjini Shinyanga.
Askofu Potts amesema baadhi ya watu wamekuwa wakitoa
jumbe zisizo sahihi, hivyo ni muhimu kwa waumini kuchunguza kila wanachokisikia
kwa kukilinganisha na maandiko matakatifu huku akisisitiza kuwa kila ujumbe
unaozua mashaka unapaswa kuthibitishwa kupitia Biblia.
“Maandiko yanasema watu wangu wanaangamia
kwa kukosa maarifa. Hii ina maana wengi wanaopotoshwa hawana uelewa wa kutosha
wa neno la Mungu,” amesema.
Ameongeza kuwa kanisa halijabadilika, bali mabadiliko
yapo kwa baadhi ya watu wanaokengeuka kutoka katika misingi ya imani, huku
akiwahimiza waumini kuendelea kuwa na matumaini kwa Mungu katika nyakati zote.
Awali akifungua ibada hiyo, Mchungaji wa Kanisa la
AICT Kambarage, Charles Lugembe, aliwataka Wakristo kuendelea kumshukuru Mungu
kwa amani iliyopo nchini Tanzania, akieleza kuwa hali hiyo imewezesha uhuru wa
kuabudu kuendelea kudumu.
Aidha, amewahimiza waumini kuendelea kuliombea taifa
ili kudumisha umoja na mshikamano.
Kwa upande wake, Mchungaji mstaafu Amos Ndaki ametumia
nafasi hiyo kuwaombea viongozi wa serikali akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Waziri Mkuu na viongozi
wengine, ili waendelee kuliongoza taifa kwa hekima, amani na utulivu.
Ibada hiyo pia imehudhuriwa na Askofu wa AICT Dayosisi ya Shinyanga, Askofu Zakayo Bugota, huku ikipambwa na uimbaji kutoka kwa kwaya mbalimbali zikiwemo AIC Kambarage Choir, kwaya ya vijana, AIC Shinyanga pamoja na kwaya ya akina mama.

Askofu wa AICT Dayosisi ya Shinyanga, Askofu Zakayo
Bugota, akizungumza kwenye ibada ya leo Jumapili katika Kanisa la AICT Kambarage. 
Mchungaji wa Kanisa la AICT Kambarage, Charles Lugembe, akiongozi ibada
ya leo Jumapili.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Kambarage, Charles Lugembe, akiongozi ibada ya leo Jumapili.

Askofu Carlton Potts kutoka Texas, Marekani, akihubiri
katika ibada ya leo Jumapili kwenye kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga.

Askofu Carlton Potts kutoka Texas, Marekani, akihubiri
katika ibada ya leo Jumapili kwenye kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga.
Katibu wa kanisa la AICT Kambarage, Maligisa James Dotto akisoma matangazo ya kanisa kwenye ibada ya leo Jumapili Aprili 12, 2026.
Katibu wa kanisa la AICT Kambarage, Maligisa James Dotto akisoma matangazo ya kanisa kwenye ibada ya leo Jumapili Aprili 12, 2026.
AIC Kambarage Choir, wakiimba katika ibada ya leo
Jumapili.












































































Post a Comment