Na Mapuli Kitina Misalaba
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yanayoendelea katika
uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
yameendelea kushika kasi ambapo timu ya KIMANDAGULI FC (KUNGULU WEUSI) imeibuka na ushindi wa
mabao 3-1 dhidi ya KASHISHI FC katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa na
kuvutia mashabiki wengi waliojitokeza kushuhudia burudani ya soka.
Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano
Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mechi zinazofuata huku akiendelea
kuwakumbusha wananchi wa jimbo la Solwa pamoja na maeneo jirani kujitokeza kwa
wingi katika uwanja wa Mwabenda kushuhudia michezo hiyo inayozidi kuleta
burudani na kuibua vipaji vya vijana.
Amesema mechi ya kesho ni timu ya ISENENGEJA
itamenyana na MWAKITOLYO No.6 katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani
mkubwa ndani ya uwanja wa Mwabenda.
Amesema mashindano hayo yanaendelea kuwa jukwaa muhimu
la kukuza michezo pamoja na kuimarisha mshikamano wa jamii kupitia soka.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na
Bwana Paul Daud Augustino kupitia ufadhili wa Lushu Foundation kwa lengo la
kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo pamoja na kuhamasisha mshikamano
miongoni mwa wananchi.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Timu ya Kashishi FC
Wachezaji wa KIMANDAGULI na KASHISHI FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa leo Mei 24, 2026.
Wachezaji wa KIMANDAGULI na KASHISHI FC wakioneshana ushindani mkubwa katika mchezo wa NIACHEKONA CUP 2026 uliochezwa uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa leo Mei 24, 2026.
Viongozi pamoja na wadau wa michezo wakifuatilia ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 kupitia mchezo wa leo ambao umewakutanisha KIMANDAGULI na KASHISHI FC.
Wachezaji wa KIMANDAGULI wakishangilia moja ya mabao yao katika mchezo wa ushindani mkubwa dhidi ya KASHISHI FC.
Mchezo ukiendelea ambapo KIMANDAGULI iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KASHISHI FC leo Mei 24, 2026.
Mchezo ukiendelea ambapo KIMANDAGULI iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KASHISHI FC leo Mei 24, 2026.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

























Post a Comment