
Mwalimu Richard Makoye (wa tatu kutoka kulia) akiongoza kikao cha tathmini ya matokeo ya mtihani wa pamoja kwa shule za sekondari za Manispaa ya Shinyanga, kilicholenga kuimarisha taaluma na ufaulu wa wanafunzi.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga,
Richard Makoye, ametoa wito kwa walimu, wanafunzi na wadau wa elimu kuimarisha
umoja na mshikamano ili kuinua kiwango cha elimu na kudumisha amani katika
jamii.
Makoye ameyasema hayo leo Aprili 21, 2026 wakati
akiongoza kikao cha tathmini ya matokeo ya mtihani wa pamoja wa mwezi Aprili,
kilicholenga kuchambua maendeleo ya taaluma na kuweka mikakati ya kuboresha
ufaulu kwa wanafunzi wa shule za sekondari.
Kikao hicho kilihusisha jumla ya shule 31 kutoka
Manispaa hiyo, kikiwa na washiriki 112 wakiwemo Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa
Shule, Makamu Wakuu wa Shule pamoja na walimu wa taaluma.
Akizungumza katika kikao hicho, Makoye amesema
mafanikio ya elimu hayawezi kupatikana bila ushirikiano, akisisitiza kuwa
walimu wanapaswa kufanya kazi kwa umoja, nidhamu na kujituma ili kuwajengea
wanafunzi msingi imara wa kitaaluma na maadili mema.
“Tunataka kuona mabadiliko chanya katika matokeo ya
wanafunzi, hivyo ni muhimu kwa walimu na viongozi wa elimu kushirikiana
kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati iliyowekwa,” amesema Makoye.
Makoye pia ametoa rai kwa walimu kuendelea kuwa mlezi
bora wa wanafunzi si tu katika taaluma bali pia katika kuwajenga kiakili na
kimaadili, ili waweze kuwa raia wema watakaolinda amani ya taifa.
Kwa ujumla, kikao hicho kimeweka msisitizo katika kujenga mshikamano miongoni mwa wadau wa elimu, kikilenga kuhakikisha kuwa mazingira ya kujifunzia yanakuwa ya amani, salama na yenye tija kwa maendeleo ya wanafunzi na taifa kwa ujumla.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




















Post a Comment