" MWENYEKITI CCM KATAVI AFANYA ZIARA KATA 27 MPANDA, ASISITIZA UMOJA NA UHAI WA CHAMA

MWENYEKITI CCM KATAVI AFANYA ZIARA KATA 27 MPANDA, ASISITIZA UMOJA NA UHAI WA CHAMA

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi, Iddi Hassan Kimanta, amekamilisha ziara ya siku saba katika kata zote 27 za Wilaya ya Mpanda iliyofanyika kuanzia Aprili 9 hadi 15, 2026, akikutana na wanachama na viongozi wa ngazi mbalimbali.

Katika ziara hiyo, Kimanta alilenga kuwasalimia wanachama, kuwashukuru kwa ushindi mkubwa wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuhimiza mshikamano katika kukijenga chama. Alisema mafanikio yaliyopatikana yanatokana na umoja, juhudi na ushirikiano wa wanachama katika ngazi zote.

Aidha, aliwataka wanachama kuendelea kuimarisha uhai wa chama kwa kulipa ada na kusajili wanachama wapya, huku akizihimiza jumuiya zake za Umoja wa Vijana wa CCM, Umoja wa Wanawake wa Tanzania na wazazi kuongeza kasi ya uhamasishaji katika maeneo yao.

Katika hatua nyingine, Kimanta aliahidi kutoa vyeti vya shukrani kwa kila kata kama ishara ya kuthamini mchango wa wanachama katika kuimarisha chama na kuleta ushindi. Pia aliwataka wanachama kuendeleza upendo, amani na mshikamano bila kujali nafasi au cheo.

Ziara hiyo pia ilitumika kuwapongeza madiwani, wabunge na viongozi mbalimbali wa mkoa huo kwa ushirikiano wao, huku akitolea mfano mafanikio ya kupatikana kwa mbunge wa tatu wa viti maalum mkoani Katavi.

Akizungumza na wanachama katika kata mbalimbali, Kimanta alisisitiza umuhimu wa kujenga mahusiano mazuri ndani ya chama, kusikiliza na kutatua kero za wanachama pamoja na kusonga mbele katika utekelezaji wa majukumu ya chama bila kukwama.

Katika hitimisho la ziara hiyo, alielekeza viongozi wa ngazi za matawi, mashina, kata na wilaya kuhakikisha wanatoa mafunzo kwa wanachama, kufanya vikao vya mara kwa mara, kuandika kumbukumbu sahihi, kubuni miradi ya maendeleo na kuimarisha nidhamu pamoja na mawasiliano ndani ya chama.

Ziara hiyo ilihusisha kata zote 27 za Wilaya ya Mpanda, zikiwemo Kashaulili, Majengo, Misunkumilo, Kakese, Ibindi, Katumba, Mtapenda na Ugalla, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha chama katika ngazi ya msingi.


SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post