Na Mapuli Kitina Misalaba
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi (SACP), amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani na
kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha usalama wa raia na
mali zao unaimarika.
Akizungumza kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa
Aprili leo 28, 2026, Kamanda Magomi amesema ushirikiano kati ya wananchi na
vyombo vya ulinzi na usalama ni silaha muhimu katika kupambana na vitendo vya
uhalifu vinavyojitokeza katika jamii.
Amesema mafanikio yaliyopatikana katika operesheni
mbalimbali zilizofanywa mkoani humo yanatokana na ushirikiano huo, huku
akisisitiza kuwa juhudi zaidi zinahitajika ili kudhibiti uhalifu na kulinda
amani iliyopo.
Kamanda Magomi amebainisha kuwa Jeshi la Polisi
linaendelea kuchukua hatua madhubuti dhidi ya wahalifu na wale wote wanaokiuka
sheria, na kuwataka wananchi kutoa taarifa mapema pindi wanapobaini viashiria
vya uhalifu katika maeneo yao.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa wananchi kufuata sheria
na taratibu za nchi, akieleza kuwa kufanya hivyo kutasaidia kujenga mazingira
salama na yenye utulivu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kutoa wito kwa jamii kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani, kwa kushirikiana na mamlaka husika ili kuifanya Shinyanga kuwa sehemu salama kwa wote.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment