" SAIDA KAROLI ATAMANI KUFANYA KAZI NA ALI KIBA, DIAMOND PLATNUMZ HAKUNILIPA PESA YOYOTE

SAIDA KAROLI ATAMANI KUFANYA KAZI NA ALI KIBA, DIAMOND PLATNUMZ HAKUNILIPA PESA YOYOTE

Msanii mkongwe wa muziki wa asili Saida Karoli amefunguka kwa hisia kali katika kipindi cha Misalaba Media, akieleza maumivu aliyopitia baada ya kumpoteza mama yake, hatua iliyomtikisa kisaikolojia na kumfanya kupoteza mwelekeo wa maisha kwa kipindi fulani.

Pia Saida mbali na Mama yake amesema baada ya Ruger kufariki, alijihisi kupoteza kila kitu kwani alikuwa nguzo muhimu katika maisha na kazi yake ya muziki. Kutokana na hali hiyo, aliamua kurudi kijijini na kujitenga na tasnia, huku akidai kuwa hata mawasiliano na wasanii wenzake yalikatika kabisa.

Aidha, Saida aligusia changamoto nyingine ikiwemo madai ya kuzushiwa mahusiano na bosi wake yaliyomuumiza zaidi, pamoja na kueleza namna muziki unavyomchanganya kihisia anapokuwa peke yake.

Pia amedai kuwa msanii Diamond Platnumz aliwahi kuwasiliana naye kuomba kutumia wimbo wake wa Salome, lakini baadaye wimbo huo ulitoka bila makubaliano ya kifedha.

Licha ya kuitwa Malkia wa muziki wa asili, Saida amesema bado anakabiliwa na maisha magumu, na amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumsaidia kupata bendi yake ya muziki.

Hata hivyo, ameweka wazi ndoto yake ya kufanya kazi na Ali Kiba, hasa kwa kuurudia upya wimbo wake maarufu wa Salome.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post