" VIONGOZI WA DINI SHINYANGA WAHIMIZA WAUMINI KULINDA AMANI NA KULIOMBEA TAIFA

VIONGOZI WA DINI SHINYANGA WAHIMIZA WAUMINI KULINDA AMANI NA KULIOMBEA TAIFA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Viongozi wa dini katika Kanisa la AICT Kambarage, mkoani Shinyanga, wamewataka waumini kuendelea kudumisha amani na kuliombea taifa ili kuimarisha umoja na mshikamano wa Watanzania.

Akifungua ibada hiyo, Mchungaji wa Kanisa la AICT Kambarage, Charles Lugembe, amewataka Wakristo kumshukuru Mungu kwa amani iliyopo nchini, akieleza kuwa hali hiyo imewezesha uhuru wa kuabudu kuendelea kudumu bila vikwazo.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa waumini kuendelea kuliombea taifa ili kudumisha hali ya utulivu na mshikamano, huku akibainisha kuwa amani ni tunu inayopaswa kulindwa na kila Mtanzania.

Kwa upande wake, Mchungaji mstaafu Amos Ndaki ametumia nafasi hiyo kuwaombea viongozi wa serikali akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Waziri Mkuu na viongozi wengine, ili waendelee kuliongoza taifa kwa hekima, amani na utulivu.

Ibada hiyo pia ilihudhuriwa na Askofu wa AICT Dayosisi ya Shinyanga, Askofu Zakayo Bugota, na kupambwa na uimbaji wa kwaya mbalimbali zikiwemo AIC Kambarage Choir, kwaya ya vijana, AIC Shinyanga pamoja na kwaya ya akina mama.

Kwa pamoja, viongozi hao wa dini wamehimiza jamii kuendelea kuthamini na kulinda amani iliyopo nchini kama msingi wa maendeleo na ustawi wa taifa.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post