Na Edington Mukiza Ezron, Misalaba Media
Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Shinyanga
wametakiwa kuwaombea viongozi wa taifa pamoja na kuendelea kudumisha amani,
upendo na mshikamano nchini.
Rai hiyo imetolewa leo Mei 27, 2026 na Sheikh wa Mkoa
wa Shinyanga, Sheikh Ismail Habibu Makusanya, wakati wa swala ya Eid Al-Adha
iliyofanyika katika uwanja wa Saba Saba uliopo kata ya Kambarage Mjini
Shinyanga.
Sheikh Makusanya amesema Waislamu wanapaswa kuwaombea
viongozi wao akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita, pamoja na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa
viongozi hao wamekuwa wakifanya kazi ya kuwatumikia wananchi kwa karibu.
Amesema ni muhimu kwa waumini kuendelea kufanya dua
kwa Mwenyezi Mungu ili viongozi wawe na afya njema, hekima na uwezo wa
kuendelea kuliongoza taifa katika misingi ya amani na maendeleo.
Aidha, amewahimiza wananchi kuendelea kudumisha amani
nchini kwa kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha migogoro na kuvuruga
mshikamano wa kitaifa, huku akisisitiza umuhimu wa umoja na upendo katika
jamii.
Katika hatua nyingine, Sheikh Habibu ametoa wito kwa
waendesha vyombo vya moto kuzingatia sheria na usalama barabarani wakati wa
maadhimisho ya sikukuu ya Eid Al-Adha, ili kuepusha ajali zinazoweza
kuhatarisha maisha ya wananchi.
Pia amewasisitiza madereva wa bodaboda kuepuka kubeba
abiria zaidi ya mmoja maarufu kama “mishikaki”, akisema hatua hiyo itasaidia
kulinda usalama wa wananchi na kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Sheikh Ismail Habibu
Makusanya, akiongoza swala ya Eid Al-Adha katika uwanja wa Saba
Saba Manispaa ya Shinyanga leo Mei 27, 2026.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Sheikh Ismail Habibu
Makusanya, akiongoza swala ya Eid Al-Adha katika uwanja wa Saba
Saba Manispaa ya Shinyanga leo Mei 27, 2026.
Waumini wa dini ya Kiislamu wakishiriki swala ya Eid kwa pamoja leo Mei 27, 2026 mkoani Shinyanga.



























Post a Comment