" UKOSEFU WA AJIRA NA MAKUNDI RIKA VYACHOCHEA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA SHINYANGA

UKOSEFU WA AJIRA NA MAKUNDI RIKA VYACHOCHEA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA SHINYANGA

Na Milu Malimi, Misalaba Media

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Shinyanga wameeleza wasiwasi wao juu ya kuongezeka kwa matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana, wakisema hali hiyo inaathiri kwa kiasi kikubwa ustawi wa maisha yao na maendeleo ya jamii.

Wakizungumza na Misalaba Media Mei 1, 2026, wananchi hao wamesema matumizi ya dawa za kulevya yamechangia kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu ikiwemo uporaji, unyanyasaji wa watoto pamoja na kuvunjika kwa familia, huku vijana wengi wakijikuta wakiingia katika makundi hatarishi na kushawishiwa na marafiki wabaya.

Miongoni mwa waliozungumza ni Abdallah Rajabu, Hamis Hasan, Devotha Mfoi na Kitenge Chubwa, ambao wameeleza kuwa ukosefu wa ajira umeendelea kuwa sababu kubwa inayowasukuma baadhi ya vijana kujiingiza katika matumizi ya dawa hizo, sambamba na ushawishi wa makundi rika yanayowavuta kwenye vitendo vya kihalifu kama ujambazi na ukabaji.

Wamesisitiza kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuimarisha malezi kwa kuwafuatilia watoto wao kwa karibu na kujenga mazingira ya mawasiliano ya wazi, ili vijana waweze kueleza changamoto wanazokutana nazo kabla ya kuathirika na matumizi ya dawa za kulevya.

Aidha, wamezitaka shule na taasisi mbalimbali kuongeza juhudi za utoaji elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya, huku wakihimiza jamii kuwajengea vijana uwezo kupitia mafunzo ya ujasiriamali na fursa nyingine za maendeleo ili waweze kujitegemea.

Kwa upande mwingine, wananchi hao wameitaka jamii kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa kuhusu wahusika wa biashara haramu ya dawa za kulevya, wakiamini hatua hiyo itasaidia kujenga mazingira salama na kulinda nguvu kazi ya taifa.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post