" WAFUKUNYUNGU FC KUTOKA MJINI SHINYANGA YAIBUKA NA USHINDI DHIDI YA MWASENGE KWENYE NIACHEKONA CUP 2026

WAFUKUNYUNGU FC KUTOKA MJINI SHINYANGA YAIBUKA NA USHINDI DHIDI YA MWASENGE KWENYE NIACHEKONA CUP 2026


Na Mapuli Kitina Misalaba

Ligi ya NIACHEKONA CUP 2026 inayoendelea katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imeendelea kushika kasi huku timu ya Wafukunyungu FC kutoka mjini Shinyanga ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo wa leo dhidi ya Mwasenge kutoka kata ya Salawe.

Mashindano hayo ambayo yameanza rasmi Mei 16, 2026 yanashirikisha jumla ya timu 22 kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga ikiwemo Mkoa wa Mwanza, Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Geita, Manispaa ya Shinyanga pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga jimbo la Solwa.

Katibu wa kamati ya mashindano hayo amesoma ratiba ya mechi za kesho ambapo DUARA FC watamenyana na MWANDUTU huku akiwahimiza wananchi na wadau wa michezo kujitokeza kwa wingi kuendelea kushuhudia burudani ya soka pamoja na vipaji vya vijana vinavyoendelea kuoneshwa katika mashindano hayo.

Kwa upande wake mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud maarufu MC NIACHEKONA amesema mshindi wa kwanza katika ligi hiyo atazawadiwa zaidi ya shilingi milioni moja na nusu pamoja na kombe, huku mshindi wa pili akitarajiwa kupata shilingi laki sita na mshindi wa tatu laki tatu.

Aidha amesema kutakuwa na zawadi mbalimbali kwa timu na wachezaji watakaofanya vizuri ikiwemo timu yenye nidhamu, mchezaji bora pamoja na golikipa bora wa mashindano hayo.

Mbali na michezo, MC NIACHEKONA ni Meneja wa Kishushu Hotel na pia ni mchimba madini katika mgodi wa Mwakitolyo. Kwa huduma za MC NIACHEKONA wasiliana naye kupitia namba 0757 267 738.

RATIBA YA MECHI – NIACHEKONA CUP 2026

Mei 16, 2026
HOME BOYS Vs MANHEIGANA

Mei 17, 2026
WAFUKUNYUNGU FC Vs MWASENGE

Mei 18, 2026
DUARA FC Vs MWANDUTU

Mei 19, 2026
SHILIMA Vs SONGAMBELE MHANGU

Mei 20, 2026
NYUNDO FC Vs NZOZA

Mei 21, 2026
MAHEMBE Vs MAWEMIRU

Mei 22, 2026
NYANDOLWA Vs BAJAJ FC

Mei 23, 2026
SHILABELA Vs LYABUKANDE

Mei 24, 2026
KIMANDAGULI Vs KASHISHI

Mei 25, 2026
ISENENGEJA Vs MWAKITOLYO No.6

Mei 26, 2026
SANGU FC Vs BULIGE

Mazoezi kabla ya mechi

 Kwa taarifa zote, matokeo ya mechi, ratiba pamoja na matukio mbalimbali ya NIACHEKONA CUP 2026, endelea kufuatilia Misalaba Media kupitia kurasa zake zote za mitandao ya kijamii.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post