Na Mapuli Kitina Misalaba
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Paschal
Patrobas Katambi, amewataka viongozi wa dini nchini kuendelea kuhubiri amani,
upendo na maadili mema ili kulinda umoja wa taifa, akieleza kuwa mmomonyoko wa
maadili umekuwa tishio kubwa kwa ustawi wa Tanzania kuliko hata janga la
UKIMWI.
Mhe. Katambi ameyasema hayo leo Juni 28 alipokuwa mgeni
rasmi akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu
Hassan, katika ibada ya uchangiaji wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki
mwa Ziwa Victoria, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Shinyanga.
Akizungumza mbele ya waumini na viongozi mbalimbali wa
dini na serikali, Waziri Katabi amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ina jukumu la
kuhakikisha usalama wa wananchi, kulinda amani na kusimamia utekelezaji wa
sheria, lakini juhudi hizo haziwezi kufanikiwa bila ushirikiano wa viongozi wa
dini.
Ameeleza kuwa Tanzania imeanza kushuhudia dalili za
kuporomoka kwa maadili ya jamii, hali ambayo inaweza kuhatarisha mshikamano na
amani ya nchi ikiwa haitadhibitiwa mapema.
Waziri Katambi ameongeza kuwa baadhi ya watu wamekuwa
tayari kuchochea vurugu na machafuko kwa ajili ya kupata madaraka au maslahi
binafsi, hali inayotishia amani ambayo Tanzania imeijenga kwa miaka mingi.
Aidha, ameeleza kuwa Serikali imebaini uwepo wa
kampeni mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii zinazowashawishi vijana kujiunga
na vikundi vinavyohamasisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Amesema serikali pia imekuwa ikifuatilia na kuchukua
hatua dhidi ya watu wanaosambaza video na ujumbe unaochochea uharibifu wa
shule, majengo ya serikali na miundombinu ya umma pamoja na kuhamasisha vitendo
vya uhalifu.
Pamoja na hayo, Waziri Katambi amesema Serikali ya Rais
Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira bora ya malezi kwa watoto
na vijana ili kujenga kizazi chenye maadili, uzalendo na uwajibikaji.
Kwa upande wake, Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kusini
Mashariki mwa Ziwa Victoria, Dkt. Yohana Nzeru, amesema kanisa linaendelea
kuthamini ushirikiano uliopo kati yake na serikali katika kuwahudumia wananchi
na kujenga jamii yenye maadili.
Ujenzi wa shule hiyo unatarajiwa kuongeza fursa za elimu bora kwa watoto wa Shinyanga na maeneo jirani, huku ukilenga kuwalea katika misingi ya elimu, maadili na hofu ya Mungu.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Paschal Patrobas Katambi
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254









Post a Comment