Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Nyandolwa FC imefanikiwa kutinga hatua ya robo
fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa
penati dhidi ya Shilabela FC katika mchezo uliochezwa leo Juni 10, 2026 kwenye
Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa.
Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulimalizika
kwa sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 za kawaida, hali iliyolazimu
mshindi kupatikana kwa mikwaju ya penati kwa mujibu wa kanuni za mashindano
hayo.
Katika hatua ya mikwaju ya penati, Nyandolwa FC
ilionesha utulivu na umakini mkubwa kwa kufunga penati zake tatu za mwanzo,
huku Shilabela FC ikikosa penati zote tatu za awali na hivyo kushindwa
kuendelea na mashindano hayo.
Ushindi huo umeifanya Nyandolwa FC kufuzu rasmi hatua
ya robo fainali huku safari ya Shilabela FC katika mashindano ya NIACHEKONA CUP
2026 ikifikia tamati.
Baada ya mchezo huo, viongozi wa Shilabela FC
wameushukuru uongozi wa mashindano pamoja na mwandaaji kwa kuwapa nafasi ya
kushiriki. Aidha, wameomba Kamati ya Mashindano kuzingatia uwezekano wa
kurejeshwa kwa nafasi ya “Best Rooza” ili kutoa fursa kwa baadhi ya timu
zilizoondolewa kuendelea kushiriki katika hatua za baadaye.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi Jilya, ametangaza ratiba ya mchezo wa
kesho ambapo Bulige FC itamenyana na Manheigana FC katika pambano
linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikisaka nafasi ya
kutinga hatua inayofuata.
Sambayi Jilya amewahimiza wananchi, wadau wa michezo
na mashabiki kuendelea kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda
kushuhudia michezo mbalimbali inayoendelea kuibua vipaji vya vijana na
kuimarisha mshikamano wa jamii.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana
Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu
Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo,
kuimarisha amani na mshikamano wa jamii.
Kwa mawasiliano ya shughuli mbalimbali za kijamii,
michezo, matangazo na ushereheshaji wa matukio, wasiliana na MC NIACHEKONA
kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Shilabela FC.
Kikosi cha Nyandolwa FC.
Waamuzi wa mechi.
Wachezaji wa Nyandolwa FC na Shilabela FC wakioneshana ushindani mkubwa katika pambano la kusaka tiketi ya robo fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.
Wachezaji wakipambana kutafuta bao la ushindi kabla ya hatima ya mchezo kuamuliwa kwa mikwaju ya penati.
Wadau wa michezo na uongozi wa mashindano ukifuatilia mwenendo wa mchezo huo huku ukiendelea kusimamia utekelezaji wa kanuni za NIACHEKONA CUP 2026.

Mashabiki wakifuatilia kwa hamasa kubwa mchezo kati ya Nyandolwa FC na Shilabela FC uliomalizika kwa mikwaju ya penati leo Juni 10, 2026.

Mashabiki wakifuatilia kwa hamasa kubwa mchezo kati ya Nyandolwa FC na Shilabela FC uliomalizika kwa mikwaju ya penati leo Juni 10, 2026.

Mashabiki wakifuatilia kwa hamasa kubwa mchezo kati ya Nyandolwa FC na Shilabela FC uliomalizika kwa mikwaju ya penati leo Juni 10, 2026.
Burudani ya soka ikiendelea katika Uwanja wa Mwabenda huku kila timu ikisaka ushindi wa kusonga mbele kwenye mashindano hayo.
Burudani ya soka ikiendelea katika Uwanja wa Mwabenda huku kila timu ikisaka ushindi wa kusonga mbele kwenye mashindano hayo.
Dakika 90 za ushindani mkali zikishuhudiwa kati ya Nyandolwa FC na Shilabela FC katika mchezo uliovuta hisia za mashabiki wengi.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
















Post a Comment