Na Mapuli Kitina Misalaba
Mabingwa watetezi wa mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026,
Sangu FC kutoka Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, wamefanikiwa kutinga hatua ya
timu 12 bora baada ya kuiondoa Bulige FC kutoka Wilaya ya Kahama mkoani
Shinyanga kwa faida ya mabao ya jumla katika michezo miwili.
Katika mchezo wa marudiano uliochezwa leo Jumamosi
Juni 6, 2026 katika Uwanja wa Mwabenda
kata ya Solwa Mkoani Shinyanga, timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2 katika
pambano lililokuwa na ushindani mkubwa kuanzia dakika za mwanzo hadi mwisho.
Matokeo hayo yanaifanya Sangu FC kuendelea na
mashindano hayo kutokana na faida waliyoipata katika mchezo wa kwanza ambapo
waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Bulige FC.
Kwa kujumlisha matokeo ya michezo yote miwili, Sangu
FC imefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3 (aggregate) na hivyo
kujihakikishia nafasi ya kucheza hatua ya timu 12 bora huku safari ya Bulige FC
katika mashindano hayo ikifikia tamati.
Kwa upande wao, viongozi wa Bulige FC wamemshukuru
mwandaaji wa mashindano hayo kwa kuwapa nafasi ya kushiriki huku wakiahidi
kurejea kwa nguvu zaidi katika mashindano yajayo.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano, Sambayi Jilya, amesema kuanzia kesho Jumapili mashindano yataingia
rasmi katika hatua ya timu 12 bora ambapo michezo itachezwa kwa mfumo wa mtoano
wa moja kwa moja, timu itakayofungwa ikiondolewa mara moja kwenye mashindano
hayo.
Baadhi ya michezo iliyopangwa kuchezwa katika hatua ya
timu 12 bora ni pamoja na:
Nyundo FC dhidi ya
Mawemiru FC, Duara FC dhidi ya Songambele Mhangu FC na Home Boys FC dhidi ya
Ufukunyungu FC
Ameendelea kuwakaribisha wananchi, wadau wa michezo na
mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda kushuhudia
michezo ya hatua hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa zaidi.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na mdau
wa michezo Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la
Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani
na kukuza michezo katika jamii.
Kwa mawasiliano ya Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli
mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia
namba 0757 267 738.
NIACHEKONA CUP MWABENDA – WEKA TU WEKE.
Kikosi cha Bulige FC na kocha wa timu.
Wachezaji wa Sangu FC na Bulige FC wakioneshana uwezo mkubwa katika pambano la kusaka tiketi ya timu 12 bora.
Mchezo ukiendelea kwa ushindani mkubwa huku kila timu ikisaka ushindi muhimu.
Viongozi wa mashindano wakifuatilia kwa karibu mchezo kati ya Sangu FC na Bulige FC.
Wadau wa michezo na viongozi wa jamii wakishuhudia vipaji vya vijana vinavyoendelea kuibuliwa kupitia NIACHEKONA CUP 2026.
Watangazaji wa mechi.
Mashabiki wa soka wakifuatilia kwa hamasa kubwa pambano kati ya Sangu FC na Bulige FC katika Uwanja wa Mwabenda.
Mashabiki wa soka wakifuatilia kwa hamasa kubwa pambano kati ya Sangu FC na Bulige FC katika Uwanja wa Mwabenda.
Mashabiki wa soka wakifuatilia kwa hamasa kubwa pambano kati ya Sangu FC na Bulige FC katika Uwanja wa Mwabenda.
Wachezaji wa timu zote mbili wakionesha ari ya ushindani katika mchezo uliojaa burudani kwa mashabiki.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254


























Post a Comment