" SONGAMBELE MHANGU FC YATINGA ROBO FAINALI BAADA YA KUIONDOA DUARA FC NIACHEKONA CUP 2026

SONGAMBELE MHANGU FC YATINGA ROBO FAINALI BAADA YA KUIONDOA DUARA FC NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba


Timu ya Songambele Mhangu FC imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Duara FC katika mchezo mkali uliochezwa leo Jumatatu Juni 8, 2026 katika uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Bao pekee la ushindi katika mchezo huo lilifungwa na Masanja Kabelele katika dakika ya sita ya mchezo, bao ambalo lilidumu hadi filimbi ya mwisho na kuipa Songambele Mhangu FC tiketi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata ya mashindano hayo.

Licha ya Duara FC kufanya jitihada mbalimbali za kutafuta bao la kusawazisha, safu ya ulinzi ya Songambele Mhangu FC ilisimama imara na kufanikiwa kulinda ushindi huo muhimu.

Kutokana na matokeo hayo, safari ya Duara FC katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 imefikia tamati. Viongozi wa timu hiyo wameushukuru uongozi wa mashindano pamoja na mwandaaji kwa kuwapa nafasi ya kushiriki, huku wakikiri kuwa hawakufanikiwa kufikia malengo waliyojiwekea msimu huu.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Mashindano ya NIACHEKONA CUP ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo Home Boys FC kutoka Kata ya Solwa watamenyana na Ufukunyungu FC kutoka Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga, katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashindano hayo, Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA, amewashukuru wananchi na wadau wa michezo kwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kufuatilia mechi mbalimbali zinazochezwa kila siku katika uwanja wa Mwabenda.

Amesema mwitikio mkubwa wa wananchi unaonesha kuwa mashindano hayo yamekubalika na yanaendelea kutimiza lengo la kuibua vipaji vya vijana pamoja na kutoa burudani kwa jamii.

Aidha, amewahimiza wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kushuhudia vipaji vya vijana na watoto wao wanaoshiriki katika mashindano hayo.

Sambamba na hilo, MC NIACHEKONA ameielekeza Kamati ya Mashindano kuendelea kusimamia kwa umakini kanuni na taratibu zilizowekwa ili kuhakikisha mashindano yanaendeshwa kwa haki, amani na nidhamu.

Amesisitiza kuwa hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya timu au watu watakaokiuka kanuni za mashindano hayo ili kulinda hadhi ya ligi na kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata burudani katika mazingira ya amani na utulivu.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha mshikamano wa jamii na kukuza michezo katika Mkoa wa Shinyanga na maeneo jirani.

Kwa huduma za ushereheshaji wa matukio mbalimbali, matangazo na burudani, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha Songambele Mhangu FC.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




 

Post a Comment

Previous Post Next Post