Na Mapuli Kitina Misalaba
Mafundi nchini wamehimizwa kuendelea kuwa mabalozi wa
amani na mshikamano katika jamii, wakielezwa kuwa mazingira ya amani na utulivu
ndiyo msingi wa maendeleo ya sekta ya ujenzi na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
Wito huo umetolewa katika semina maalumu iliyoandaliwa
na kampuni ya MAGIC BUILDERS, iliyofanyika katika Ukumbi wa Lyakale, Manispaa
ya Shinyanga, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe.
Paschal Patrobas Katambi.
Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Katambi amesema
Serikali haitakuwa tayari kuruhusu kundi dogo la watu wenye maslahi binafsi
kuvuruga amani ya nchi kwa kujificha nyuma ya misingi ya haki za binadamu na
demokrasia.
Amesema Serikali itaendelea kuhakikisha hali ya
usalama na utulivu inaendelea kuimarika nchini ili Watanzania waendelee kufanya
shughuli zao za kiuchumi kwa uhuru na amani.
Katika hatua nyingine, Katambi amewataka waajiri
kuwathamini mafundi kwa kuwalipa stahiki zao kwa wakati na kwa mujibu wa
makubaliano waliyoingia.
Amesema Serikali haitamvumilia mtu au taasisi yoyote
itakayowadhulumu mafundi kwa kutowalipa fedha walizokubaliana baada ya
kukamilisha kazi zao.
Pia amewahimiza mafundi kufanya kazi kwa uadilifu,
kuzingatia viwango vya taaluma pamoja na kuhakikisha wanatumia mikataba rasmi
wanapopewa kazi ili kulinda maslahi yao na ya waajiri.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa MAGIC BUILDERS, David
Barongo, amesema kampuni hiyo imeamua kuandaa semina hiyo ikiwa ni sehemu ya
kuwajengea uwezo mafundi na kuwapa elimu kuhusu haki zao, wajibu wao pamoja na
namna ya kujenga kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyokubalika.
Amesema mafundi ni nguzo muhimu katika maendeleo ya
sekta ya ujenzi, hivyo wanapaswa kuendelea kupata mafunzo ya mara kwa mara ili
kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira.
Barongo ameongeza kuwa kampuni hiyo, kwa kushirikiana
na Serikali, imeandaa mpango maalumu wa kuwatambua na kuwarasimisha mafundi
ambao bado hawana vyeti vya taaluma.
Amesema kupitia ushirikiano huo, mafundi hao
watapatiwa mafunzo na fursa ya kupata vyeti vya taaluma bila malipo kupitia
Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga.
Kwa mujibu wa Barongo, zoezi hilo la usajili, tathmini
na utoaji wa mafunzo litafanyika kwa siku mbili kuanzia Jumanne, Julai 21,
2026, likiwa na lengo la kuongeza idadi ya mafundi wenye sifa na wanaotambulika
rasmi nchini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth
Magomi, amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika
kulinda na kudumisha amani, akisisitiza kuwa usalama ni jukumu la kila
mwananchi.
Amesema kila mtu ana haki ya kufanya kazi, kuendesha
biashara na kutekeleza shughuli zake za kila siku katika mazingira ya utulivu
na usalama, hivyo ni muhimu kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga amani.
Kuhusu masuala ya maandamano, Kamanda Magomi amesema
shughuli hizo zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za
nchi, huku akiwataka wananchi kutoshiriki vitendo vya uchochezi au uvunjifu wa
sheria vinavyoweza kuhatarisha usalama wa watu na mali zao.
Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kusimamia
utekelezaji wa sheria kwa haki na weledi ili kuhakikisha Mkoa wa Shinyanga
unaendelea kuwa salama na wananchi wanaendelea na shughuli zao za maendeleo
bila hofu.
Baadhi ya mafundi walioshiriki semina hiyo
wameishukuru kampuni ya MAGIC BUILDERS pamoja na Serikali kwa kuandaa mafunzo
hayo, wakisema yatawaongezea ujuzi, kuimarisha taaluma zao na kuongeza fursa za
ajira.
Wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uaminifu
na kuzingatia maadili ya taaluma huku wakilinda amani ambayo ndiyo msingi wa
maendeleo ya sekta ya ujenzi na Taifa kwa ujumla.
Semina hiyo ilihitimishwa kwa burudani kutoka kwa
wasanii mbalimbali wakiwemo mchekeshaji Ndaro, pamoja na TX Dullah, Kidege na
Azaboi, ambao wametoa burudani iliyowavutia washiriki wa semina hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, akizungumza na mafundi katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS mjini Shinyanga
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, akizungumza na mafundi katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS mjini Shinyanga
Mkurugenzi wa kampuni ya MAGIC BUILDERS, David Barongo, akieleza dhamira ya kampuni hiyo ya kuwawezesha mafundi kupitia mafunzo ya kuongeza ujuzi, kuwarasimisha na kuwapatia vyeti vya taaluma kwa kushirikiana na Serikali pamoja na Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya MAGIC BUILDERS, David Barongo, akieleza dhamira ya kampuni hiyo ya kuwawezesha mafundi kupitia mafunzo ya kuongeza ujuzi, kuwarasimisha na kuwapatia vyeti vya taaluma kwa kushirikiana na Serikali pamoja na Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi, akitoa elimu kwa washiriki wa semina kuhusu wajibu wa kila mwananchi katika kulinda amani, kuzingatia sheria na kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha mazingira salama ya kazi na maendeleo yanaendelea kudumu.
Washiriki wa semina wakifuatilia mada mbalimbali zilizolenga kuongeza ujuzi wa kazi, matumizi ya mikataba, uaminifu katika utekelezaji wa miradi pamoja na umuhimu wa kulinda amani kwa maendeleo ya sekta ya ujenzi.
Washiriki wa semina wakifuatilia mada mbalimbali zilizolenga kuongeza ujuzi wa kazi, matumizi ya mikataba, uaminifu katika utekelezaji wa miradi pamoja na umuhimu wa kulinda amani kwa maendeleo ya sekta ya ujenzi.
Mamia ya mafundi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo yaliyotolewa katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS, yenye lengo la kuwajengea uwezo, kuimarisha taaluma na kuhamasisha uzingatiaji wa sheria na maadili ya kazi.
Mamia ya mafundi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo yaliyotolewa katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS, yenye lengo la kuwajengea uwezo, kuimarisha taaluma na kuhamasisha uzingatiaji wa sheria na maadili ya kazi.
Mamia ya mafundi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo yaliyotolewa katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya MAGIC BUILDERS, yenye lengo la kuwajengea uwezo, kuimarisha taaluma na kuhamasisha uzingatiaji wa sheria na maadili ya kazi.
Mmoja wa mafundi wenye bahati akikabidhiwa pikipiki kama zawadi maalumu kutoka kampuni ya MAGIC BUILDERS, ikiwa ni sehemu ya kutambua juhudi, kuwahamasisha mafundi na kuongeza ari ya kufanya kazi kwa bidii na ubora.
Mmoja wa mafundi wenye bahati akikabidhiwa pikipiki kama zawadi maalumu kutoka kampuni ya MAGIC BUILDERS, ikiwa ni sehemu ya kutambua juhudi, kuwahamasisha mafundi na kuongeza ari ya kufanya kazi kwa bidii na ubora.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
































































Post a Comment