" TAFITI ZINAZOFANYWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA TAIFA

TAFITI ZINAZOFANYWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA TAIFA



 Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.

........................ 

TAFITI zinazofanywa na Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), zimekuwa na mchango mkubwa katika Taifa hasa katika kuanzishwa kwa sheria mpya.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.

‘’ Tafiti tunazozifanya zina mchango mkubwa katika taifa kwani baadhi zimeleta sheria na nyingine zilileta vifungu katika sheria,” alisema Chanzi.

Alisema hapo awali maendeleo ya kidijitali yalikuwa siyo makubwa lakini yalipokuja Tume hiyo ilifanya tafiti mwaka 2005 ambayo ilizaa sheria mbili, sheria ya miamala ya kielektroniki na makosa ya kimtandao.

“Hatukuwa na sheria hizo hivyo baada ya utafiti tulipendekeza Serikalini na ilitunga hizo sheria na ndiyo maana tunaona watu wana udhubutu wa kutuma hela kwa njia ya kimtandao bila ya kuwa na wasiwasi wowote kwa kuwa wanajua zipo sheria,” alisema Chanzi. 

Alisema mwaka 2020 Tume hiyo ilifanya tafiti kuhusiana na ulinzi wa taarifa binafsi kutokana na kuwa na umuhimu wake kama ambavyo zinavyolindwa katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema katika kuendana na kidijitali Tume imetekeleza wajibu wake na inaendelea na utekelezaaji huo ambapo kwa sasa inafanya utafiti wa Akili Mnemba (AI)  na hayo yote ni mapinduzi yay a kidijitali na wao kama tume wanazifanya tafiti hizo na kuishauri Serikali iweze kuchukua hatua zinazofaa kulingana na jamii yetu.

Chanzi aliongeza kuwa wanaendelea kufanya tafiti na wanapozikabidhi sheria zimekuwa zikitungwa jambo ambalo wanajivunia.

“Tafiti tunazo zifanya siyo tu za kidijitali kwa mfano tulifanya teknolojia ya DNA ambayo zamani ilikuwa haipo lakini Tume ilifanya tafiti na kukabidhi ripoti na sheria ikatungwa na kwa kuwa tulikuwa na teknolojia lakini bila ya kuiwekea sheria ya kuisimamia ingeweza kusababisha yasipatikane matokeo chanya ambayo yangehitajika.

Chanzi amesema misingi ambayo waliiweka kwenye ripoti zao wameweza kuiona ipo ndani ya sheria na kuonesha jinsi gani mapendekezo wanayotoa yanavyochukuliwa na kufanyiwa kazi.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post