
Mwenyekiti mpya wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania
(TRCS) Mkoa wa Shinyanga, Hatibu Madata Mgeja, amekabidhiwa rasmi ofisi pamoja
na mali za taasisi hiyo, ikiwa ni hatua ya kuanza rasmi majukumu yake baada ya
kuchaguliwa kuongoza chama hicho mkoani Shinyanga.
Makabidhiano hayo yamefanyika leo Agosti 17, 2026
katika Ofisi za TRCS Mkoa wa Shinyanga, ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa Red
Cross Mkoa wa Shinyanga, Robert Kayoka, amekabidhi ofisi na mali za taasisi kwa
Mwenyekiti mpya.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mwenyekiti
mpya, Hatibu Madata Mgeja, amesema amepokea dhamana hiyo kwa heshima na
atashirikiana na viongozi, wanachama, Serikali pamoja na wadau mbalimbali
katika kuimarisha shughuli za Chama cha Msalaba Mwekundu Mkoa wa Shinyanga.
Mgeja amesema uongozi wake utalenga kuimarisha
ushirikiano na wadau pamoja na kuhakikisha shughuli za chama zinawafikia
wananchi wenye uhitaji, huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano katika
kutekeleza majukumu ya kibinadamu.
Makabidhiano hayo yamehitimisha rasmi kipindi cha uongozi wa Robert Kayoka na kufungua ukurasa mpya wa uongozi chini ya Mwenyekiti Hatibu Madata Mgeja, ambaye anatarajiwa kuendelea kuimarisha utendaji na huduma za Chama cha Msalaba Mwekundu Mkoa wa Shinyanga.
Makabidhiano rasmi ya Ofisi na Mali za Red Cross Mkoa wa Shinyanga, ambapo Mwenyekiti mpya Hatibu Madata Mgeja (kulia) akikabidhiwa rasmi ofisi na mali za taasisi na aliyekuwa Mwenyekiti Robert Kayoka.

Mwenyekiti mpya wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS) Mkoa wa
Shinyanga, Hatibu Madata Mgeja
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



















Post a Comment