" SHIRIKA LA YAWE LATUNUKIWA CHETI KWA UTUNZAJI WA MAZINGIRA KATIKA MANISPAA YA SHINYANGA

SHIRIKA LA YAWE LATUNUKIWA CHETI KWA UTUNZAJI WA MAZINGIRA KATIKA MANISPAA YA SHINYANGA

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imelipatia cheti Shirika la Youth and Women Emancipation (YAWE) kwa kutambua mchango wake katika shughuli za utunzaji na uhifadhi wa mazingira.

Cheti hicho kimetolewa kwa YAWE ikiwa ni miongoni mwa wadau wanaofanya vizuri katika kuhamasisha na kutekeleza shughuli zinazolenga kulinda mazingira katika Manispaa ya Shinyanga.

Cheti hicho kimekabidhiwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wazo Marco Mwang’onda, mara baada ya hafla ya uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia unaotekelezwa kata ya Ndembezi.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Wazo Marco Mwang’onda ameupongeza uongozi wa YAWE kwa jitihada za kushiriki katika shughuli za utunzaji wa mazingira, akisisitiza umuhimu wa wadau kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na changamoto za uharibifu wa mazingira.

Amesema matumizi ya nishati safi ya kupikia ni miongoni mwa hatua muhimu katika kulinda mazingira, kupunguza utegemezi wa nishati zinazochangia uharibifu wa misitu na kuboresha afya za wananchi.

Mwakilishi wa shirika la  YAWE Bwana Peter Joseph ameishukuru Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kutambua mchango wa shirika hilo, huku ukieleza kuwa cheti hicho ni motisha ya kuendelea kuimarisha shughuli za utunzaji wa mazingira na kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi.

Hatua hiyo imekuja wakati ambapo Mwenge wa Uhuru 2026 ukiendelea na shughuli zake mkoani Shinyanga, ukiwa na kauli mbiu inayosema: “Tanzania ni yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo.”

Peter Joseph, mwakilishi wa Shirika la Youth and Women Emancipation (YAWE), akiwa upande wa kulia, akipokea cheti kwa niaba ya shirika hilo kutoka kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wazo Marco Mwang’onda, kwa kutambua mchango wa YAWE katika utunzaji wa mazingira Shinyanga.

  

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post