
Tamasha la Kizimkazi lililofanyika Zanzibar limetajwa kuwa jukwaa muhimu la kukuza umoja, mshikamano wa kitaifa, na udugu wa kudumu miongoni mwa Watanzania huku likiimarisha tunu ya Muungano .
Akizungumza kufuatia kufungwa kwa tamasha hilo, Mtaalam wa Maridhiano, Amani na Maendeleo, Dkt. Dennis Muchunguzi, aliwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za maendeleo ili kuchochea malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kulinda amani ya nchi.
Aidha, aliongeza kuwa uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania Bara na Zanzibar una mizizi mirefu hata kabla ya Muungano, akitolea mfano wa mchezo wa soka kati ya timu za Simba na Yanga uliochezwa visiwani humo kama ushahidi wa mshikmano huo imara unaopaswa kulindwa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Dkt. Muchunguzi amesisitiza kuwa mshikamano wa kitaifa ni msingi muhimu wa utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050, hususan katika juhudi za kuinua uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment