" ZAWADI ‘MAHONA CUP – 12’ ZABORESHWA, TIMU 30 KUCHUANA KUWANIA MILIONI 5 NA KOMBE

ZAWADI ‘MAHONA CUP – 12’ ZABORESHWA, TIMU 30 KUCHUANA KUWANIA MILIONI 5 NA KOMBE

 

 

Mkurugenzi wa 'MAHONA CUP – 12', Patrick Mahona, akizungumza wakati wa ufunguzi wa MAHONA CUP - 12' uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Segese katika Halmashauri ya Msalala, wilayani Kahama mkoani Shinyanga, yakilenga kuibua vipaji vya soka.

Mkurugenzi wa 'MAHONA CUP – 12', Patrick Mahona ametangaza kuongeza viwango vya zawadi kwa timu zitakazoshiriki ligi hiyo na kuibuka mshindi wa 1 – 4.

 

Amefafanua kuwa mshindi wa kwanza sasa atapata zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni tano (5,000,000) pamoja na kombe, mshindi wa pili atapata fedha taslimu shilingi milioni 2.5, mshindi wa tatu atapata shilingi laki tano na wa nne kusalia na mipira miwili.

 

“Tumeboresha viwango vya zawadi kwa mshindi wa kwanza mpaka wa tatu, lkini mshindi wan ne amebaki kwenye mipira. Nisisitize kwamba hapa bado sio mwisho, zawadi zinaweza kubadilika na kuboreshwa zaidi wakati wowote.” Amesema Mahona ambaye pia ni dwani wa kata ya Segese

 

Na kuongeza “Kuna mdau ameguswa na ligi akaongeza dau, kwa hiyo tuendelee kuifatilia ‘MAHONA CUP’ mambo mazuri yanakuja kwa vijana wetu, vipaji vipo, na tunachotaka ni kuviibua sisi ngazi ya jamii ili ngazi za juu zione na kuviendeleza.”

 

Hata hiyo mkurugenzi huyo ameahidi pia kutoa zawadi kwa mchezaji bora, mfungaji bora pamoja na kijana atakayeshiriki ligi akiwa na umri mdogo zaidi.

 

‘MAHONA CUP’ imezinduliwa rasmi leo Agosti 26, 2026, katika viwanja vya shule ya msingi Segese katika Halmashauri ya Msalala, wilayani Kahama mkoani Shinyanga, yakilenga kuibua na kuwasaidia vijana wenye ndota za kucheza soka kutimiza ndoto zao.

 

Katika mechi ya ufunguzi hii leo imekutanisha Itinde U20 Fc na uton Fc zote kutokea kata ya segese ambapo Luton Fc imeibuka mshindi kwa kuichapa Itinde U20 goli 5 kwa 2, hivyo Itinde U20 inafungua dimba la kuyaaga mashindano haya muhimu kwa ukuaji wa vipaji vya vijana.

 

HATUA YA MTOANO

 

Mechi ya ufunguzi Agosti 26, 2026 ni kati ya Itinde Fc na Luton Fc, Agost 27, 2026 ni kati ya Supertiger Fc na Chemichemi Fc. Agost 28, 2026 ni kati ya Kilimanjaro Fc na Imani Academy, Agost 29, 2026 ni kati ya Mlimani Fc na Newboys Ntobo. Agost 30, 2026 ni kati ya MAHONA Boys na Veterans Fc.

  

Endelea kutufuatilia…..














Post a Comment

Previous Post Next Post