" 𝗭𝗔𝗜𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝟭,𝟯𝟬𝟬 𝗪𝗔𝗦𝗛𝗜𝗥𝗜𝗞𝗜 𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝟮𝟬𝟮𝟲 𝗞𝗔𝗦𝗨𝗟𝗨 𝗠𝗝𝗜, 𝗪𝗔𝗛𝗜𝗠𝗜𝗭𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗔 𝗪𝗔𝗭𝗔𝗟𝗘𝗡𝗗𝗢, 𝗞𝗨𝗟𝗜𝗡𝗗𝗔 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗖𝗛𝗔𝗡𝗚𝗔𝗠𝗞𝗜𝗔 𝗙𝗨𝗥𝗦𝗔 𝗭𝗔 𝗞𝗜𝗨𝗖𝗛𝗨𝗠𝗜

𝗭𝗔𝗜𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝟭,𝟯𝟬𝟬 𝗪𝗔𝗦𝗛𝗜𝗥𝗜𝗞𝗜 𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝟮𝟬𝟮𝟲 𝗞𝗔𝗦𝗨𝗟𝗨 𝗠𝗝𝗜, 𝗪𝗔𝗛𝗜𝗠𝗜𝗭𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗔 𝗪𝗔𝗭𝗔𝗟𝗘𝗡𝗗𝗢, 𝗞𝗨𝗟𝗜𝗡𝗗𝗔 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗖𝗛𝗔𝗡𝗚𝗔𝗠𝗞𝗜𝗔 𝗙𝗨𝗥𝗦𝗔 𝗭𝗔 𝗞𝗜𝗨𝗖𝗛𝗨𝗠𝗜


Zaidi ya vijana 1,300 wameshiriki Kongamano la Vijana 2026 la Halmashauri ya Mji Kasulu lenye lengo la kuwaunganisha vijana kujadili masuala ya uraia, fursa za kiuchumi, changamoto mbalimbali wanazokutana nazo na njia bora ya kuzitatua kwa faida na manufaa  yao na Taifa kwa ujumla.Kongamano hilo limefanyika Septemba 05, 2026 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu (Kasulu TTC) na kuwakutanisha vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo.Akifungua kongamano hilo, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Isaac Anthony Mwakisu amewataka vijana kujishughulisha, kuwa wazalendo, kulinda amani na kutumia vyema fursa zilizopo katika kujenga maisha yao na kuunga mkono juhudi zote za Serikali katika kuchochea maendeleao.Aidha, Kanali Mwakisu amewahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wa Uhuru unaotarajia kuwasili Halmashauri ya Mji Kasulu Septemba 10, 2026. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Mwl. Vumilia Julius Simbeye amewataka vijana kuendelea kuuunga mkono juhudi za Serikali, kuketi na kujadili namna ya kupata suluhisho la changamoto zinazowakabili kwa kushiriki makongamano na vikao vinavyowahusu.Naye Amina Kaniki, mwakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, amewahimiza vijana kutumia teknolojia kwa tija ili kujenga uchumi wao na kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana.Kongamano hilo limejikita kujadili mada  mbalimbali  zikiwemo Uraia, Uzalendo, Amani, Uwajibikaji, Uadilifu, fursa za kiuchumi, mikopo, mitaji, biashara na fursa za uwezeshaji kwa vijana.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post