" PSSSF YAWAHIMIZA WANACHAMA KUHAKIKI TAARIFA ZAO MAPEMA

PSSSF YAWAHIMIZA WANACHAMA KUHAKIKI TAARIFA ZAO MAPEMA

Na Mapuli Misalaba

Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umewahimiza wanachama kutumia mifumo ya kidijitali kuhakiki taarifa za michango na mafao yao mapema ili kubaini makosa na kuepuka changamoto wakati wa kudai mafao.

Wito huo umetolewa leo, Septemba 18, 2026, mjini Shinyanga wakati wa semina ya PSSSF kwa waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari za Shinyanga na Simiyu pamoja na Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN).

Akizungumza katika semina hiyo, Afisa Msimamizi wa PSSSF Mkoa wa Simiyu, Salum Mwegelo, amesema wanachama wanapaswa kufuatilia taarifa zao mara kwa mara badala ya kusubiri hadi wanapokaribia kustaafu.

Aidha, Mwegelo amewataka wastaafu kuwa makini na watu wanaojitambulisha kama mawakala wa PSSSF, akisisitiza kuwa mfuko huo hauna mawakala wanaotoa huduma kwa niaba yake.

Amesema wastaafu wanapaswa kutumia njia rasmi za PSSSF na kutotoa taarifa za siri, ikiwemo namba za siri za akaunti zao, kwa watu wasiokuwa na mamlaka.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Mfawidhi PSSSF Shinyanga, Sunday Rashid, amesema mfuko umeanza kushughulikia taarifa za watumishi wanaokaribia kustaafu miezi sita kabla ya tarehe yao rasmi ya kustaafu ili kutoa muda wa kuhakiki taarifa na kurekebisha changamoto.

Naye Mratibu wa TBN Kanda ya Ziwa, Kadama Malunde, amewasisitiza waandishi wa habari kutumia taaluma yao kuwafikishia wananchi elimu sahihi kuhusu haki, wajibu na huduma za hifadhi ya jamii.

Amesema waandishi na wanablogu wana wajibu wa kuhakikisha taarifa wanazozifikisha kwa umma zinathibitishwa, zina usahihi na zina manufaa kwa jamii.

Afisa Msimamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Mkoa wa Simiyu Salum Mwegelo akizungumza.
Mratibu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) Kanda ya Ziwa Kadama Malunde akizungumza kwenye mafunzo hayo kwa niaba ya Mwenyekiti wa (TBN) Beda Msimbe.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga Greyson Kakuru akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Makamu Mwenye wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu Paschal Michael akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Afisa Uhusiano kutoka PSSSF Abdul Njaidi akizungumza katika mafunzo hayo.





TAZAMA PICHA NA MARCO MADUHU👇👇
Afisa Msimamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Mkoa wa Simiyu Salum Mwegelo akizungumza.
Afisa Uhusiano kutoka PSSSF Abdul Njaidi akizungumza katika mafunzo hayo.
Afisa Mahusiano na Mtoa elimu kwa wanachama PSSSF Flora Sumari, akizungumza katika mafumo hayo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga Greyson Kakuru akizungumza kwenye mafunzo hayo.

Post a Comment

Previous Post Next Post